Thursday 2 April 2015

SHAMBULIO LA CHUO KIKUU KENYA 'LAUA 147'



A Kenyan soldier escorts a woman after she was rescued

Idadi ya watu waliouawa katika shambulio lililofanywa na al-Shabab kwenye chuo kikuu kaskazini-mashariki mwa Kenya imeongezeka kufikia 147, maafisa wa serikali walisema.

Harakati za kijeshi za kudhibiti chuo kikuu cha Garissa sasa zimekwisha, huku washambuliaji wote wanne wakiwa wameuawa, walisema.

Maafisa walisema wanafunzi 587 walitolewa, 79 wakiwa wamejeruhiwa.

Sheria ya kupigwa marufuku kutoka usiku inatekelezwa katika baadhi ya sehemu nchini humo.

Kaunti nne katika mpaka wa Kenya-Somalia, Garissa, Wajir, Mandera na Tana River, wamezuia watu kutoka nje siku nzima.

Wanafunzi tisa waliojeruhiwa vibaya sana walisafirishwa kwa ndege kwenye mji mkuu Nairobi kwa matibabu.

Kwa maelezo zaidi, bonyeza link ifuatayo
http://bbc.in/1DrBXQW

No comments:

Post a Comment