Tuesday 31 March 2015

MUHAMMADU BUHARI ASHINDA NIGERIA



File photo: Goodluck Jonathan (left) and Muhammadu Buhari shake hands after signing a peace deal agreeing to respect the outcome of the polls
Goodluck Jonathan (kushoto) na Muhammadu Buhari walikubaliana wiki iliyopita kuheshimu matokeo ya uchaguzi

Aliyekuwa kiongozi wa kijeshi Muhammadu Buhari amekuwa mgombea wa kwanza wa upinzani kushinda uchaguzi wa urais Nigeria.

Chama cha Jenerali Buhari kimesema mpinzani wake, Goodluck Jonathan, alikubali kushindwa na kumpa pongezi.

Bw Jonathan alipishana na Jenerali Buhari kwa takriban kura milioni mbili alipogoma mara ya kwanza kukubali kushindwa.

Waangalizi kwa ujumla wameusifia uchaguzi lakini kumekuwa na madai ya udanganayifu, ambao baadhi wanahofia kunaweza kusababisha maandamano na ghasia.

Kwa taarifa zaidi, bonyeza link ifuatayo

http://www.bbc.co.uk/news/world-africa-32139858

BUHARI 'ANAONEKANA' KUONGOZA UCHAGUZI NIGERIA



People watch election news coverage on television at a street in Lagos, Nigeria, 30 March 2015

Matokeo ambayo bado hayajakamilika kutoka uchaguzi wa Nigeria unaashiria aliyekuwa kiongozi wa kijeshi Muhammadu Buhari amepata kura zaidi kuliko rais wa sasa aliye madarakani, Goodluck Jonathan.

Hata hivyo, majimbo yenye watu wengi zaidi kama vile Lagos na Rivers bado matokeo hayakutangazwa rasmi.

Huku nusu tu ya majimbo ya Nigeria yakiwa yametangazwa, chama cha Jenerali Buhari cha All Progressives Congress (APC) kiliripotiwa kuwa na kura zaidi kwa milioni mbili.

Matokeo zaidi yanatarajiwa kutangazwa siku ya Jumanne.

Tume ya uchaguzi ya Nigeria (Inec) ilisitisha kutangaza matokeo Jumatatu usiku, baada ya kutoa matokeo ya majimbo 18 na mji mkuu Abuja.

Chama cha Rais Jonathan cha People's Democratic Party (PDP) kilipata kura 6,488,210 na cha APC cha Jenerali Buhari kimepata kura 8,520,436.

                                                                                                                                                                                        

Monday 30 March 2015

MWENDESHA MASHTAKA WA UGANDA AUAWA



Security checks in Kampala, 26 March
Ulinzi uliimarishwa baada ya onyo la shambulio la ugaidi

Joan Kagezi, mwendesha mashtaka mkuu wa Uganda katika kesi ya watu 13 walioshutumiwa kwa shambulio kubwa la bomu la al-Shabab, amepigwa risasi na kufariki dunia mjini Kampala.

Bi Kagezi alilengwa na watu wenye silaha waliokuwa kwenye pikipiki alipokuwa njiani akielekea nyumbani.

Shambulio la bomu la kujitoa mhanga la mwaka 2010 Kampala lilisababisha vifo vya watu 76 walipokuwa wakitazama fainali ya Kombe la Dunia.

Wiki iliyopita, ubalozi wa Marekani Uganda iliwaonya raia wote wa kigeni – wakiwemo Wamarekani – uwezekano wa kulengwa na mashambulio ya “kigaidi” mjini Kampala.

Bi Kagezi, wakili mwandamizi, aliongoza idara ya umma ya kuzuia ugaidi na pia idara ya uhalifu wa kivita.

Msemaji wa polisi wa Kampala Patrick Onyango alisema: "Walikuwa wakimfuatilia na pikipiki – walimpiga risasi na kumwuua.


UCHAGUZI NIGERIA: MATOKEO YA AWALI YATARAJIWA



An official of the Independent National Electoral Commission retrieves on March 29, 2015 documents from ballot boxes from the presidential election

Tume ya kusimamia uchaguzi Nigeria imesema inatarajia kutangaza matokeo ya awali ya uchaguzi wa Rais siku ya Jumanne baada ya raia wa nchi hiyo kupiga kura Jumamosi.

Rais aliye madarakani Goodluck Jonathan anakabiliwa na changamoto nzito kutoka kwa aliyekuwa kiongozi wa kijeshi Muhammadu Buhari.

Umoja wa mataifa umeusifia upigaji kura huo licha ya kuwepo hitilafu za kiufundi, maandamano na ghasia yanayohusishwa na Boko Haram

Upigaji kura uliendelea mpaka siku ya pili katika baadhi ya sehemu nchini Nigeria baada ya kuwepo matatizo ya mfumo mpya wa kutumia kadi za kielektroniki.

 

Sunday 29 March 2015

KINYESI KUPITA KIASI MLIMA EVEREST



 Mount Everest

Kinyeshi kupita kiasi na mikojo huachwa ikijazana na wapanda mlima kwenye mlima Everest.

Jambo hilo linasababisha uchafuzi wa mazingira na huenda ukaeneza maradhi, alisema mkuu wa jumuiya ya wapanda mlima wa Nepal.

Ang Tshering anataka serikali ya Nepal kuwaambia wageni wote kuhifadhi uchafu huo  inavyostahili.

Alisema kinyesi na mikojo imekuwa “ikijazana” kwa miaka kadhaa maeneo ya kambi nne zilizopo.

“Wapandaji milima huchimba shimo kwenye theluji kama vile choo na kuacha uchafu huo hapo.”

Zaidi ya wapanda mlima 700 na wanaowaongoza hukaa takriban miezi miwili mlimani humo kila msimu, ambapo huanza mwanzoni mwa mwezi Machi na kumalizika mwezi Mei.

Baadhi ya wapanda milima hubeba mifuko maalum ya kuhifadhi uchafu huo kwenye kambi za juu zaidi, alisema.

Kwenye kambi za chini kuna maturubali maalum ndio kama vyoo, ambapo ina njia maalum ya kupitisha uchafu huo.

Serikali ya Nepal bado inatafuta suluhu ya tatizo hilo.

Sheria mpya zinamaanisha kuwa kila mpanda mlima lazima arudi na kilo 8 za uchafu wanaporudi chini.

Hicho ni kiwango ambacho wataalamu wanaamini mpanda mlima hutoa akiwa safarini.

Watu hao pia hulipa dola 4000, ambazo hawarudishiwi  kama watashindwa kutimiza masharti hayo.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

Friday 27 March 2015

FILAMU KUHUSU ALBINO YAZINDULIWA LONDON

   
 Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko kubwa la mauaji ya albino, hasa katika mataifa ya Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Tanzania na vile vile Burundi. Watu hao hulengwa kutokana na itikadi za kichawi kwa madai kuwa viungo vyao huleta utajiri, bahati na kuponyesha maradhi yoyote. Filamu moja inayoangazia mauaji ya albino Tanzania 'White Shadow' imezinduliwa London wiki hii, Zuhura Yunus wa BBC alihudhuria uzinduzi huo.

HIV: DHARURA YA KIAFYA KUTANGAZWA INDIANA



Computer artwork of the HIV virus

Gavana wa Indiana ametangaza dharura ya afya ya umma baada ya mlipuko wa HIV “kufikia kiwango cha kusambaa” sehemu ya jimbo hilo.

Kaunti ya Scott, eneo la kimaskini ambapo watumiaji wa dawa za kulevya kutumia sindano moja kwa pamoja si jambo la ajabu, ambapo katika wiki za hivi karibuni maambukizi mapya 79 yameongezeka kutoka wastani wa watu watano.

 Gavana Mike Pence ameidhinisha maafisa wa afya kutekeleza mradi wa kutoa elimu juu ya kubadilishana sindano – jambo alilowahi kukataa siku za nyuma.

HIV ni kirusi kinachosababisha ugonjwa wa Aids.

Mlipuko huo mwanzo ulitambuliwa mwezi Januari mwishoni. Tangu wakati huo, maafisa wamegundua watu 79 wakiwa na ugonjwa huo – kutoka watu 26 tu mwezi uliopita.