Tuesday 28 October 2014

RWANDA YAFANYA VYEMA USAWA WA KIJINSIA





Ushiriki wa wanawake zaidi katika siasa na kazi nyingine imepunguza idadi ya utofauti wa kijinsia duniani katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, Jukwaa la Kiuchumi Duniani (WEF) limesema.

Utafiti wa mwaka wa jinsia wa WEF umethibitisha “mabadiliko makubwa” katika nchi nyingi, huku nchi 105 zikiwa na usawa tangu mwaka 2005, mwandishi wa ripoti hiyo amesema.

Iceland ndio inaongoza kwa miaka sita mfululizo, huku Yemen ikishikilia mkia.

WEF imeangazia zaidi uchumi, afya, elimu na ushiriki wa kisiasa katika nchi 142.

Mataifa sita tu - Sri Lanka, Mali, Croatia, Macedonia, Jordan na Tunisia – yameshuhudia usawa wa kijinsia kuongezeka kwa ujumla tangu mwaka 2005, kulingana na WEF.

Moja ya sababu za mafanikio ya Iceland ni idadi ndogo ya watu nchini humo wakati Yemeni ina idadi kubwa ya vifo na watoto wengi wa kike wenye umri wa miaka sita hadi 14 hawajawahi kuhudhuria shule

Rwanda yafanya vyema

Mataifa ya Nordic yanaongoza, huku Finland, Norway na Sweden yanaifuata Iceland katika tano bora.

Uingereza imeshuka kwa nafasi nane duniani na kufikia nafasi ya 26.

Rwanda imeingia katika orodha hiyo kwa mara ya kwanza na kuchukua nafasi ya saba, na kuifanya nchi yenye mafanikio makubwa kiuchumi barani Afrika.

Mwandishi wa ripoti hiyo Saadia Zahidi alisema mafanikio ya Rwanda ni kwasababu kuna karibu idadi sawa ya wanawake na wanaume wenye ajira – na katika ofisi za wizara – na badala yake huduma za afya na elimu zimeimarika.

Mabadiliko ya mapato ya wanawake ndio iliyoiporomosha Uingereza, ilisema WEF.

Msukosuko wa uchumi ndio umesababisha utofauti wa kipato wa kijinsia kuongezeka Uingereza.

Kutaka kujua zaidi na kujua nchi yako iko nafasi ya ngapi, Bonyeza hapa

http://www.bbc.co.uk/news/world-29722848

No comments:

Post a Comment