Monday 22 September 2014

NJUGU ZILIZOKAANGWA ZINA ATHARI ZAIDI YA MBICHI

roasted peanuts
Njugu zilizokaangwa haziliwi sana Asia Mashariki, ambapo mzio wa njugu ni nadra sana kutokea huko
Njugu au karanga zilizokaangwa zina uwezekano mkubwa wa kuibua mzio (allergy) kuliko zilizo mbichi, kulingana na utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Oxford, wakihusishwa panya.

Wanasayansi wanasema mabadiliko ya kikemikali yanayosababishwa na mchakato huo wa kukaanga hubadili mfumo wa kinga wa mwili - na kuibua mzio.

Lakini utafiti zaidi unahitajika kabla watu kuamua kula njugu mbichi zaidi kuliko zilizokaangwa, walisema.

Utafiti huo unapatikana kwenye jarida la Allergy and Clinical Immunology.


Madhara makubwa

Panya walifanyiwa utafiti wa kuwekewa protini za njugu kupitia kwenye ngozi na tumboni mwao.

Wale waliopewa karanga mbichi walikuwa na kinga zaidi ya mwili - waliweza kupambana na vitu vya kigeni mwilini mwao, kuliko wale waliokula zile zilizokaangwa.

Kwa binadamu, namna kinga za mwili zinavyopambana hutofautiana. Wengine kinga zao za mwili ni za wastani na kusababisha vipele kwa mfano, lakini wengine huathirika zaidi, ambapo huvimba midomo na hata kupata matatizo ya kupumua.

Wanasayansi wanasema uwezekano mkubwa ni kutokana na jotoridi kuongezeka wakati wa kukaanga njugu ambapo husababisha mabadiliko ya kikemikali na ndipo mtu huathirika na mzio.

No comments:

Post a Comment