Saturday 27 September 2014

WACHEZA KRIKETI WAWEKA REKODI MLIMA KILIMANJARO

http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2014/09/klmm.jpg
Kupumua na kukimbia kuna uziyo kwenye sehemu hiyo ya juu

Kundi la wacheza kriketi wa kimataifa wameweka rekodi mpya ya dunia kwa kucheza mechi kubwa kwenye kilele cha Kilimanjaro, mlima mrefu zaidi Afrika, uliopo nchini Tanzania.

Timu hizo zinamhusisha mrusha mpira wa zamani wa Afrika Kusini Makhaya Ntini na mrusha mpira wa zamani wa England, Ashley Giles.

Mechi hiyo ilichezwa kwenye urefu wa mita 5,730 (futi 18,799) kwenye eneo lilinyooka chini kidogo ya kilele.
Kulikuwa na hali ya baridi na kuganda kwa barafu kwenye eneo hilo.
Kulikuwa na hali ya baridi na kuganda kwa barafu kwenye eneo hilo
        
Hii kweli maajabu! Tunacheza kriketi kwenye kilele cha Afrika, Giles alituma ujumbe kwenye Twitter.

Rekodi ya hivi karibuni ya mechi kubwa ni ile mita 5,165, iliyochezwa kwenye milima ya Himalaya, kwenye kambi ya mlima Everest nchini Nepal mwaka 2009.

Chanzo: taarifa.co.tz

No comments:

Post a Comment