Staa huyo mwenye umri wa miaka 23 alijiunga na klabu ya Arsenal akitokea katika kikosi cha Man U kwa ada ya uhamisho wa euro milioni 20 (Tsh bil 44), katika tarehe ya mwisho wa dirisha la usajili wa majira ya joto na upo uwezekano mkubwa wa kupewa nafasi ya kikosi cha kwanza mara baada ya Giroud kuumia.
Wakati huohuo kiungo wao, Aaron Ramsey anasumbuliwa na majeraha ya kifundo cha mguu ‘ankle’ aliyoyapata akiwa na kikosi cha timu ya taifa cha Wales katika mechi dhidi ya Andorra Jumanne iliyopita hivyo hatokuwepo katika mechi ya ligi kuu siku ya Jumamosi dhidi ya Man City.
Mastaa wengine wa The Gunners wanaotarajiwa kucheza dhidi ya Man City baada ya kutoka katika majeraha ni pamoja na Abou Diaby, Kieran Gibbs, Mikel Arteta, na Mesut Ozil.
Kwa upande wa Man City, Straika msumbufu , Stevan Jovetic anasumbuliwa na maumivu ya misuli ya paja ‘hamstring’ inasemekana anaweza akakosa mechi hiyo lakini mtandao wa klabu bado haujatoa taarifa za kutosha juu ya maendeleo ya staa huyo.
Jovetic mpaka sasa ametupia magoli mawili kambani katika mechi tatu alizozicheza mpaka sasa, na magoli hayo aliyapata katika mchezo dhidi ya Liverpool katika ushindi wa magoli 3-1.
Staa mwingine wa Man City ambaye yupo katika hatihati ya kucheza katika mchezo huo wa Jumamosi ni Fernando anayesumbuliwa na majeraha ya ‘groin’aliyoyapata katika mchezo wa ligi kuu walioupoteza kwa kichapo cha bao 1-0 na Stoke City.
Pia Pablo Zabaleta anaweza akaanzia benchi mara baada ya kupona majeraha aliyoyapata katika mechi ya kirafiki dhidi ya Ujerumani akiwa na kikosi chake cha Argentina.

Katika
mechi ya ligi kuu msimu uliopita wa 2013/14, Arsenal walipigwa magoli
6-3 na Man City katika mwendelezo wa rekodi mbovu za mzee Wenger dhidi
ya timu zilizopo katika ‘big-5′
Ikumbukwe mara ya mwisho kwa klabu hizi kukutana ilikuwa ni katika mchezo wa ‘Ngao ya jamii’ ambapo The Gunners waliwachapa Man City magoli 3-0 yaliyofungwa na Santi Cazorla, Ramsey na Giroud.
Tusubiri tuone kama The Gunners wataendeleza ubabe wao kwa Man City au kama kibao kitageukia upande wao.
Chanzo: taarifa.co.tz
No comments:
Post a Comment