Friday 19 September 2014

RAIS KENYATTA WA KENYA ATAKIWA ICC

Kenya's President Uhuru Kenyatta stands for Kenya's national anthem before the Africa Union Peace and Security Council Summit on Terrorism at the Kenyatta International Convention Centre in Nairobi, September 2, 2014
Kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta imewakasirisha viongozi wengi wa Afrika

Mahakama ya Kimataifa ya ICC imemtaka Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta afike katika mahakama hiyo tarehe 8 Oktoba.

Majaji wanataka kumhoji juu ya madai kuwa serikali yake imeshikilia nyaraka zinazotakiwa na waendesha mashtaka wanaoandaa kesi yake ya uhalifu dhidi ya binadamu.

Kesi hiyo tayari ishacheleweshwa mara tele.

Bw Kenyatta anakana kuhusika na mauaji ya kikabila baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.

Takriban watu 1,200 waliuawa na 600,000 kulazimika kuhama makazi yao.

Wiki mbili zilizopita, waendesha mashtaka waliomba kesi dhidi yake iahirishwe bila kutaja tarehe gani isikilizwe tena, wakisema hawana ushahidi wa kutosha kutokana na serikali ya Kenya kuchelewesha kutoa taarifa.

Rais Kenyatta amekuwa akisema mara kwa mara kuwa anahitaji kubaki Kenya ili kupambana na wapiganaji wa kundi la al-Shabab na kushughulikia masuala ya taifa.

Katika taarifa iliyotolewa, ICC imesema mazungumzo na Bw Kenyatta yatalenga " hali ya ushirikiano baina ya upande wa mashtaka na serikali ya Kenya".

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu




No comments:

Post a Comment