Tuesday 23 September 2014

WAPIGANAJI WA IS WATOA VIDEO YA PILI



 John Cantlie

Video ya pili imetolewa ikimwonyesha mwandishi wa habari wa Uingereza John Cantlie, ambaye anashikiliwa mateka na wanaojiita wapiganaji wa IS.

Tukio hilo linatokea wiki moja baada ya kutokea kwenye video kufuatia kutekwa kwake nchini Syria mwaka 2012.

Akiwa amevalishwa mavazi ya rangi ya machungwa, Bw Cantlie amesema ametelekezwa na Uingereza.

Hivi karibuni IS iliwaua mateka watatu na, kwenye video ikionyesha kifo cha mfanyakazi wa kutoa misaada wa Uingereza David Haines, na huku wakitishia kuua raia mwengine wa Uingereza Alan Henning

Ni mwandishi wa habari mwenye uzoefu mkubwa, hii ni mara ya pili kwa Bw Cantlie kutekwa Syria.

Aliwahi kutekwa Julai 2012, kufungwa pingu na kufungwa macho kwa wiki nzima, alifanikiwa kutoroka akisaidiwa na wapiganaji wanaojiita Free Syrian Army.

Video hii ya hivi karibuni imekuwa ikisambazwa huku Marekani na washirika wake wakianzisha mashambulio ya anga dhidi ya IS nchini Syria.

Majeshi ya Uingereza hayajajihusisha lakini serikali imesema huenda ikajihusisha siku za usoni.

Video hiyo ya takriban dakika sita, inafuatia mbinu zilezile za video ya kwanza akiwemo mwandishi wa habari.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment