Monday 1 December 2014

MUHAMMAD: MAARUFU KWA WATOTO WA KIUME, UK



Muhammad limekuwa jina maarufu kwa watoto wa kiume nchini Uingereza, mtandao wa BabyCentre umedai.

Wakati huohuo majina ya kiarabu yamezidi kutumika zaidi.

Vipindi vya televisheni kama vile Game of Thrones pia vimechangia sana kutoa majina ya kizazi kijacho.

Orodha ya majina 100 bora ya watoto kwa mwaka 2014 imeonyesha Muhammad imepanda nafasi zaidi ya 27 kutoka mwaka jana hadi kufika namba moja.

Jina hilo limepata nafasi hiyo baada ya kuchaguliwa na watu 56,157 wa wanachama wa mtandao wa BabyCentre.co.uk waliojifungua mwaka 2014.

Kwa ujumla kumekuwa na ongezeko kubwa la majina ya kiarabu, huku Nur likiwa jipya kuingia katika orodha hiyo katika majina 100 bora ya kike, likiruka hadi nafasi ya 29, na Maryam likipanda mara 59 na kuchukua nafasi ya 35.

Omar, Ali na Ibrahim ni majina mapya kuingia katika 100 bora za kiume.

Sophia ndio namba moja katika majina ya watoto wa kike, na kupata umaarufu tena katika orodha ya mtandao wa BabyCentre nchini Marekani, Brazil, Hispania na Urusi mwaka jana.

Lakini jina linalotamba zaidi upande wa watoto wa kike ni Maryam, huku majina mapya zaidi ni Nur, Emilia na Gracie.

Chanzo: www.theguardian.com

No comments:

Post a Comment