Friday 31 October 2014

MAUAJI YA KUTISHA DRC





Mkusanyiko wa watu ulimpiga mawe mpaka kumwuua kijana mmoja wa kiume kaskazini-mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo siku ya Ijumaa kabla ya kumchoma moto na kula maiti yake.

Mashahidi wanasema, ilikuwa ni kisasi baada ya kuwepo mfululizo wa mashambulio yaliyofanywa na waasi wa Uganda.

Tukio hilo lililotokea mjini Beni lilifuatiwa na uvamizi usiku katika eneo hilo huku wakilaumiwa kundi la ADF-NAUL, wanaodhaniwa kuwaua zaidi ya watu 100 mwezi huu, wakitumia mapanga.

Walioshuhudia walisema mtu huyo, ambaye hajatambuliwa mpaka sasa, alizua wasiwasi ndani ya basi baada ya abiria kugundua hakuweza kuzungumza lugha ya Kiswahili na alikuwa amebeba panga.

Akizungumza mjini Beni, Rais wa Congo Joseph Kabila alisema khatima ya wapiganaji wa ADF-NALU itakuwa kama ile iliyowakumba kundi la M23, lililomalizwa na jeshi linaloungwa mkono na Umoja wa Mataifa mwaka jana.

Chanzo: news.yahoo.com       
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

RAIS WA BURKINA FASO AJIUZULU





Rais wa Burkina Faso Blaise Compaore ametangaza kujiuzulu, kufuatia maandamano yenye ghasia katika jaribio lake la kuongeza uongozi wake wa miaka 27.

 Bw Compaore alitoa taarifa akisema nafasi ya rais sasa iko wazi.

Msemaji wa jeshi naye aliwaeleza waandamanaji walioshangilia sana katika mji mkuu, Ouagadougou.

Awali, waandamanaji walikasirishwa na nia yake hiyo, hivyo kuchoma moto bunge na majengo ya serikali.

Bw Compaore alisema atakabidhi madaraka baada ya serikali ya mpito kukamilisha muda wake wa miezi 12.

Katika tangazo lake la awali, Bw Compaore alitoa wito wa jeshi kutekeleza hatua za dharura za kuzingira maeneo yenye maandamano hayo.


A man stands in front of a burning car, near the Burkina Faso's Parliament where demonstrators set fire to parked cars - 30 October 2014, Ouagadougou, Burkina Faso
Waandamanaji walichoma moto magara, jengo la bunge na majengo ya serikali

Hatua hiyo ilifuatiwa na mkutano wa waandishi wa habari ambapo mkuu wa jeshi Jenerali Honore Traore alitangaza “chombo cha mpito kitaundwa kwa ushirikiano wa vyama vyote”.

Ujumbe maalum wa katikbu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon wa Afrika magharibi, Mohamed Ibn Chambas, ataelekea Burkina Faso siku ya Ijumaa katika jitihada za kutuliza mgogoro huo.

Nia yake ya kugombea tena urais ulichochea maandamano kwenye mji mkuu Ouagadougou. Maandamano hayo ni ya hatari kutokea dhidi ya uongozi wa Bw Compaore.

  • Alihudumu chini ya Rais Thomas Sankara kama waziri kiongozi
  • Alichukua madaraka baada ya Sankara kuuawa katika mazingira ya kutatanisha na kundi la askari mwaka 1987
  • Rais wa kwanza wa kuchaguliwa mwaka 1991 na 1998
  • Katiba mpya ya mwaka 2000 inatoa nafasi ya mihula miwili tu madarakani, na miaka mitano kila muhula.
  • Akashinda mihula mengine miwili ya ziada
  • Maandamano ya kupinga jaribio la kubadili muda wa mihula hiyo ilianza mwaka mmoja uliopita, ikichochewa na gharama kubwa za maisha.

MTANGAZAJI MAARUFU TZ, BEN KIKO AFARIKI DUNIA

 
Mtangazaji maarufu wa zamani wa redio Tanzania (TBC) Ben Kiko amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Oktoba 31 katika hospitali ya rufaa ya Muhimbili jijini Dar alikokuwa akipatiwa matibabu.

Ben Kiko ambaye jina lake kamili ni Ben Hamisi Kikoromo alihamishiwa katika hospitali ya jeshi ya Milambo, mkoani Tabora ambapo alilazwa kwa ajili ya matibabu ya figo kwa muda wa wiki mbili.

Mzee Kiko alijizolea umaarufu katika tasnia ya utangazaji wakati wa vita ya Kagera (Tanzania na Uganda-1979) kutokana na taarifa zake za kusisimua wakati wa mapigano hayo.

Mwaka 2012 mwanahabari huyo mkongwe alitunukiwa tuzo ya fanaka ya maisha (Lifetime Achievement Award) kutokana na mchango wake katika uandishi wa habari.

Kabla mauti hayajamfika Ben Kiko alikuwa akifanya kazi katika redio ya Voice of Tabora inayomilikiwa na Mbunge wa Tabora Mjini Ismail Aden Rage.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amin.

Chanzo: taarifa.co.tz / michuzi blog

Thursday 30 October 2014

ZAWADI YA NG'OMBE KWA BINTI KUBAKI SHULE



Schoolgirls sit around a water tank in Laikipia county in northern Kenya

Ng’ombe watatolewa kwa wazazi wa kiume kaskazini mwa Kenya iwapo watahakikisha watoto wao wa kike wanabaki shuleni, gavana wa kaunti alisema.

Gavana wa kaunti ya Laikipia, Joshua Irungu, aliiambia BBC kuwa ng’ombe tisa watatolewa kwa familia zinazoishi vijijini.

Kutokana na sheria za Kenya mzazi anayeshindwa kumpeleka mtoto wake shule ana hatari ya kufungwa gerezani.

Lakini ndoa za utotoni ni jambo la kawaida katika jamii za wafugaji, ambapo mara nyingi hutegemea na mahari ya bi harusi.

Gavana huyo ana nia ya kuanzisha kituo cha kuzalisha mifugo eneo hilo ili mradi huo uweze kudumu.

MVUTANO ISRAEL NA PALESTINA



 Israeli security forces stand behind a security perimeter outside the Menachem Begin Heritage Centre (29 October 2014)

Msemaji wa kiongozi wa Palestina Mahmoud Abbas ameelezea kufungwa kwa eneo lenye utata la sehemu takatifu la Jerusalem ni “kutangaza vita”.

Hatua hii imekuja baada ya kuwepo mvutano na vurugu kufuatia kupigwa risasi kwa mwanaharakati wa Kiyahudi.

Waziri mkuu wa Israel ametoa wito wa kuwepo utulivu, akisema Bw Abbas anachochea ghasia.

Eneo hilo takatifu litafunguliwa tena Ijumaa, waziri wa uchumi wa Israel alisema.

Yehuda Glick, mwanaharakati wa Wayahudi alijeruhiwa.

Polisi wa Israel baadae walimwuua Mpalestina anayeshukiwa kumpiga risasi mwanaharakati huyo.

Moataz Hejazi, mwenye umri wa miaka 32, alipigwa risasi baada ya kufyatua risasi alipokuta amezingirwa na polisi nyumbani kwake.

Rabbi Glick ni mwanaharakati maarufu, mzaliwa wa Marekani anayeteta haki za Wayahudi kufanya ibada kwenye eneo hilo, ambapo kwa sasa huzuiliwa.

Jengo hilo – linalojulikana kwa Wayahudi kama Temple Mount na Waislamu wanapaita  Haram al-Sharif –, ni sehemu takatifu kwa Wayahudi na pia una msikiti wa al-Aqsa  - eneo takatifu la tatu katika Uislamu.

Katika taarifa nyingine

  • Sweden imekuwa nchi ya kwanza kubwa upande wa Ulaya kuitambua rasmi Palestina kama taifa – Israel imemrejesha balozi wake wa Sweden kutokana na hilo, kulingana na afisa mmoja aliyenukuliwa na shirika la habari la AFP.
  • Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imeisihi Israel kusimamisha ujenzi wao wa makazi kwenye ukanda wa Gaza na kuchunguza madai ya ukiukwaji wa sheria unaofanywa na majeshi yake huko Gaza tangu mwaka 2008.
  • Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry alielezea madai ya kutolewa matusi na afisa mwandamizi kutoka Marekani dhidi ya Bw Netanyahu ni jambo la “aibu, lisilokubalika na lenye madhara”
Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu


GRACA ATAKA MWANAMKE KUMRITHI MUSEVENI




Uganda inatakiwa kuwa na rais mwanamke baada ya Rais Yoweri Museveni kustaafu, mke wa aliyekuwa rais wa Afrika kusini alisema.

 Mwanaharakati wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel, alisema Uganda ni miongoni mwa nchi za Afrika zenye wanawake hodari ambao wana uwezo wa kuwa rais. 

“Sijui rais Museveni ana mpango wa kustaafu lini, mwaka 2016? Sijui, lakini atakapofanya hivyo, mwanamke lazima ajiandae kuwa Rais. Ntamwambia (Museveni) tutakapokutana,”  aliyasema hayo huku akishangiliwa katika hoteli ya Serena mjini Kampala.

Machel alisikitika alipoarifiwa kuwa Dr. Specioza Wandira Kazibwe hakuwa makamu wa rais tena kwa sasa.

Rais Museveni aliweka historia alipomteua Dr. Kazibwe kuwa makamu wa rais wa kwanza Uganda mwaka 1994.

Alishikilia nafasi hiyo hadi mwaka 2003. Machel ni mjane wa aliyekuwa rais wa Afrika kusini Nelson Mandela.

Chanzo: newvision.co.ug
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu