Tuesday 28 October 2014

EBOLA: BENKI YA DUNIA YATAKA WATU KUJITOLEA



 Burial in Monrovia, Liberia, 24 Oct

Rais wa Benki ya Dunia ametoa wito kwa maelfu ya wahudumu wa afya kujitolea na kujaribu kusaidia kuzuia kuenea zaidi kwa mlipuko wa Ebola Afrika magharibi.

Jim Yong Kim alisema takriban watabibu 5,000 na wafanyakazi wengine wanahitajika kupambana na ugonjwa huo.

Wengi waliokuwa na sifa stahili wana woga wa kwenda Afrika magharibi, aliongeza.

Mlipuko wa sasa wa Ebola umewaathiri zaidi ya watu 10,000 na kuua takriban watu 5,000.

Mkuu huyo wa Benki ya Dunia Bw Kim aliyasema hayo wakati wa ziara yake nchini Ethiopia, ambapo aliungana na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon na mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Nkosazana Dlamini-Zuma.

                                                          

No comments:

Post a Comment