Thursday 30 October 2014

ZAWADI YA NG'OMBE KWA BINTI KUBAKI SHULE



Schoolgirls sit around a water tank in Laikipia county in northern Kenya

Ng’ombe watatolewa kwa wazazi wa kiume kaskazini mwa Kenya iwapo watahakikisha watoto wao wa kike wanabaki shuleni, gavana wa kaunti alisema.

Gavana wa kaunti ya Laikipia, Joshua Irungu, aliiambia BBC kuwa ng’ombe tisa watatolewa kwa familia zinazoishi vijijini.

Kutokana na sheria za Kenya mzazi anayeshindwa kumpeleka mtoto wake shule ana hatari ya kufungwa gerezani.

Lakini ndoa za utotoni ni jambo la kawaida katika jamii za wafugaji, ambapo mara nyingi hutegemea na mahari ya bi harusi.

Gavana huyo ana nia ya kuanzisha kituo cha kuzalisha mifugo eneo hilo ili mradi huo uweze kudumu.

No comments:

Post a Comment