Showing posts with label Makala. Show all posts
Showing posts with label Makala. Show all posts

Friday 5 June 2020

Ushawahi Kubaguliwa? 'Zoom na Zoo' yajadili hayo



Gumzo katika 'Zoom na Zoo'. Kutokana na ghasia zinazoendelea nchini Marekani baada dunia 

kushuhudia namna George Floyd alivyouawa na polisi kufuatia kukamatwa na kukandamizwa 

shingoni hadi pumzi zikakata, mjadala kuhusu ubaguzi wa rangi umeibuka tena. Zuhura Yunus 

kazungumza na Dan Nkurlu akiwa Marekani, Najma Said -Ujerumani, Muhammed Omar- Uingereza 

na Salim Kikeke- Uingereza. wakieleza uhalisia wa ubaguzi.



Wednesday 18 February 2015

BI HARUSI AOLEWA NA MGENI MWALIKWA KWA HASIRA


 Indian bride

Bi harusi mmoja wa India ameolewa na mmoja wa waalikwa katika harusi yake baada ya bwana harusi mtarajiwa kupatwa na kifafa na kuzimia.

Ripoti zilisema bwana harusi huyo mtarajiwa, Jugal Kishore, alikuwa na kifafa na hakumwambia mtarajiwa wake, Indira na familia ya binti huyo.

Wakati Bw Kishore alipopelekwa hospitali, bi harusi huyo mwenye hasira aliamua kutafuta  mume mbadala.

Alimwomba mmoja wa upande wa familia ya shemeji yake, aliyekuwa mwalikwa, kumwoa badala ya mtarajiwa wake. Jambo alilokubali.

Tukio hilo lilitokea mjini Rampur katika jimbo lililo kaskazini mwa India Uttar Pradesh.

Kulingana na gazeti la The Time la India, Bw Kishore, mwenye umri wa miaka 25, alianguka chini mbele ya wageni waalikwa alipotaka tu kumkamata mkono bi harusi wake Indira.

Aliporejea hospitalini, Bw Kishore alimwomba Indira abadili mawazo, akimwambia atabezwa na marafiki na ndugu zake akirudi bila mke, lakini bi harusi huyo alikataa.

Afisa polisi Ram Khiladi aliiambia BBC kuwa awali Bw Kishore na familia yake walikasirishwa na kupeleka malalamiko polisi.

"Lakini kwa kuwa bi harusi huyo kashaolewa, utafanya nini? Familia hizo zimeshatafuta suluhu na wamefuta malalamiko," aliongeza.

Monday 9 February 2015

MAMBO 5 YANAYOKWAMISHA BIASHARA



Wafanyabiashara wengi hukumbwa na changamoto nyingi katika uendeshaji wa shughuli zao za biashara. Changamoto hizi ndizo zinaweza pia kuwa utofauti wa biashara zinazokua na zile zinazokufa.

Makala hii inachambua mambo muhimu ambayo huwa ni mzigo mzito kwa wajasiriamali hata kufikia hatua ya kuathiri biashara zao, na pia makala hii inaonyesha baadhi ya njia za kukabiliana na changamoto hizo.

1. Mtaji

Kikwazo hiki hujitokeza katika mitazamo mitatu, kwanza wakati wa kutaka kuanzisha biashara, pili wakati biashara imeshaanza ila fedha hazitoshi kuendesha vema, na tatu pale mfanyabiashara anapokusudia kupanua biashara yake. Ili kukabiliana na kikwazo cha mtaji yafuatayo yanaweza kusaidia:-

Kuanza biashara kidogo kidogo: Hii namaanisha kuwa kufikiria namna ambazo unaweza kuanzisha biashara kwa mtaji mdogo na wakati huo huo ukafanya kwa ufanisi. Hii inaweza kwa kuchunguza kwa umakini gharama zisizo za lazima, mambo ambayo unaweza fanya wewe mwenyewe au kusaidia na watu wengine bila kuajiri, pia chunguza aina ya bidhaa ambazo kweli ni za lazima kuanza nazo. Kutunza taarifa za biashara yako kwa ufasaha na kuwa na muundo bora wa uongozi, hii itakusaidia kuwa kutimiza masharti ya benki, na wadau mbalimbali wa sekta ya fedha ambao wanaweza kukuongezea mtaji.

Zingatia pia kuwa na mali zisizohamishika, na pia kuna na mahusiano mazuri na wadau mbalimbali kwani wao wanaweza kuwa vyanzo vya kukupatia mtaji.

2. Muundo wa biashara

Sunday 8 February 2015

'KINYESI' CHA BINTIYE KUMWONGEZEA UZITO



Toilet paper

Mwanamke mmoja ameongezeka uzito kwa kiwango kikubwa baada ya kuhamishiwa bakteria kutoka kwenye kinyesi ‘stool transplant’ cha binti yake, madaktari walisema.

Ni utaratibu halali wa kitabibu kuhamishia bakteria wazuri kwenye utumbo ulioathirika, lakini madaktari wa Marekani wanahisi huenda imeathiri eneo la kiuno.

Ghafla aliongezeka kwa kilo 16 na sasahivi anachukuliwa kama mtu mwenye maradhi ya unene kupindukia.

Mtaalamu mmoja wa Uingereza alisema uhusiano baina ya bakteria wa tumboni na unene kupindukia bado hauko wazi.

Kuhamishiwa bacteria ‘wazuri’ wa kinyesi kwenye kiungo cha mtu mwengine hasa kwenye utumbo ‘faecal microbiota transplant’ – ambao baadhi huita "transpoosion" – kumeungwa mkono rasmi na huduma za kutoa afya za Uingereza mwaka jana.

Tiba mpya

Sunday 18 January 2015

KISWAHILI NI CHA WASIOJUA KIINGEREZA?



Katika nchi nyingi za Afrika, jamii imejigawa katika jamii ndogondogo ziitwazo makabila.

Kila kabila linakuwa na lugha inayotambulisha jamii ile. Kwa kuwa katika nchi makabila ni mengi na yanaongea lugha tofauti ambazo mara nyingi hata hazisikilizani, nchi huamua kuweka lugha moja rasmi kuwa lugha ya taifa.

Wenzetu katika nchi nyingine waliamua kuchukua lugha ya wale waliowatawala kuwa ndio lugha ya taifa. Hivyo kama walitawaliwa na Waingereza lugha ya taifa inakuwa Kiingereza, kama walitawaliwa na Wafaransa basi lugha ya taifa inakuwa Kifaransa. Tanzania ni nchi moja katika nchi chache sana katika Afrika ambazo zinatumia lugha ambazo siyo lugha za walio watawala. Sisi Tanzania tunatumia Kiswahili kama lugha ya taifa.

Mimi najivunia sana lugha hii, ninatamba mbele za walimwengu kwamba sisi tuna lugha ya Kiswahili inayotuunganisha kama taifa. Pamoja na kwamba sasa Kiswahili kimeenea sehemu nyingine za dunia hii hasa zile za Afrika Mashariki bado mimi naona hiyo ni lugha yetu sisi na wengine wamejifunza kama sisi tunavyojifunza lugha za watu wengine.

Ninaamini wapo wenye fikira kama hizi za kwangu lakini ninahisi pia wapo wanaoona lugha hii haiwahusu. Wengi wa hao ni watu wanaojua Kiingereza ambao wanaona Kiingereza ndiyo utambulisho wa usomi.

Hivyo hata kama Kiswahili kinadidimia hilo sio tatizo kwao kwani hiyo siyo lugha ya watu wenye hadhi; hata kama matumizi ya lugha hiyo ya Kiswahili siyo sahihi, hilo halijalishi kwani inakosewa lugha isiyo ya lazima kwao.

Sunday 4 January 2015

UKIPUNGUA, 'MINYAMA UZEMBE' HUENDA WAPI?

Kuwa na mwili wenye unene wa kupindukia ni tofauti na kuwa na uzito mkubwa kuliko kawaida ingawa watu wengi huchanganya mambo haya mawili na kufikiri kuwa ni jambo moja.

Unene wa kupindukia unatokana na kuwa na mafuta mengi mwilini ambayo yanasababisha mtu kuwa na nyama nyingi ambazo wengine huziita “minyama uzembe” na kitambi.

Lakini uzito mkubwa wa mwili unaweza kutokea pale mtu anapokuwa na misuli mikubwa, mifupa mikubwa, maji mengi mwilini pamoja na mafuta. Baadhi ya magonjwa na matumizi ya dawa pia yanaweza kuchagia mtu kuwa na uzito mkubwa.

Watu wenye tatizo la tezi shingo linalofanya kazi zake chini ya kiwango wanaweza kukabiliwa na tatizo hili. Matumizi ya dawa kama vile baadhi ya vidonge vya uzazi wa mpango na dawa za magonjwa ya akili, pia yanaweza kusababisha tatizo la mwili kuwa na uzito mkubwa.

Wanasayansi wa afya wamekuwa wakieleza kuwa kuna uhusiano mkubwa na wa karibu sana kati ya unene wa kupindukia na magonjwa ya moyo, kiharusi, kupanda kwa shinikizo la damu, saratani za aina mbalimbali, kisukari, kukoroma wakati wa usingizi, maumivu ya mgongo na uvimbe wa maungio yaani baridi yabisi. 
Kutokana na kupendelea kuwa na umbo la kuvutia na sababu za kiafya, watu wengi hulazimika kupunguza unene na uzito wa miili yao.

Lakini maswali ya msingi ambayo watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuhusu kupungua kwa unene wa mwili ni pamoja na njia ipi iliyo bora ya kupunguza uzito au unene?

UJAUZITO KWA NIABA - SURROGACY

Kuchukua mimba kwa niaba ni nini?

 Ni pale ambapo mwanamke anachukua ujauzito kwa nia ya kumkabidhi mtoto kwa mtu mwengine baada ya kujifungua. Kwa kifupi, anabeba ujauzito kwa ajili ya wazazi wasio na uwezo wa kuzaa – wanajulikana kama “wazazi waliokusudiwa”.

Kuna aina mbili za kuchukua mimba kwaajili ya familia nyingine. Kwa desturi, yai la mama anayebeba hiyo mimba ndilo hutumika, ambapo hubaki kuwa mama aliye na asidi nasaba zake, yaani DNA. Aina ya pili, ni pale ambapo yai linatolewa na mama ambaye anataka msaada wa mtoto au mtu aliyejitolea. Yai linarutubishwa kupitia mchakato ambao yai hurutubishwa na mbegu za kiume nje ya mwili wake yaani kwenye maabara, IVF.

Ni halali?
Ina tofauti kutoka nchi hadi nchi

Nchi kama Ufaransa, Ujerumani, Italia, Hispania, Uholanzi na Bulgaria wanakataza kabisa mfumo wa aina wowote wa kubeba mimba.
surrogate australia
Tukio la Gammy aliyezaliwa na mama aliyebeba ujauzito kwa niaba, limeleta utata Australia na Thailand
Nchi zikiwemo Uingereza, Ireland, Denmark, na Ubelgiji, ubebaji mimba kwa niaba unaruhusiwa pale ambapo mama anayebeba mimba hiyo halipwi, au hulipwa kwa matumizi maalum tu. Kumlipa mama posho (ijulikanayo kama biashara ya ubebabji mimba) ni marufuku.

Biashara ya ubebaji mimba ni halali katika baadhi ya majimbo ya Marekani, na nchi kama India, Urusi na Ukraine.

Watu wanaotaka kuwa wazazi huenda wakaenda nje ikiwa nchi zao za asili haziruhusu mchakato huo wa ubebabji mimba kwa niaba, au kama hawakufanikiwa kupata mwanamke anayeweza kuchukua mimba kwa niaba.

Hata hivyo, hata Australia sheria hubadilika. Kwa mfano, baadhi ya majimbo nchini humo ni kosa la jinai kwenda nchi nyingine kumtafuta mama atayebeba mimba kwa niaba tena kibiashara, wakati wengine huruhusu.

Watu huenda wapi kupata wa kubeba mimba kwa niaba?
Wataalamu wanasema nchi ambazo ni maarufu wa kuwa na akina mama walio tayari kuchukua mimba kwa niaba ni Marekani, India, Thailand, Ukraine na Urusi.

Mexico, Nepal, Poland na Georgia pia ni miongoni mwa nchi zinazotajwa kuwa na uwezekano wa akina mama wa kutoa huduma hizo.

Gharama zinatofautiana katika kila nchi, na pia iantegemea na idadi ya mzunguzko wa IVF unaohitajika, na iwapo bima ya afya inahitajika.
India ni maarufu kwa kutoa mama wa kuchukua ujauzito kwa niaba
India ni maarufu kwa kutoa huduma za mama wa kuchukua ujauzito kwa niaba
Families Through Surrogacy, shirika la kimataifa la kuchukua mimba kwa niaba, limekadiria wastani wa gharama za huduma hiyo katika nchi mbalimbali.
  • US - $100,000 (£60,000)
  • India - $47,350
  • Thailand - $52,000
  • Ukraine - $49,950
  • Georgia - $49,950
  • Mexico - $45,000
Kuna utata gani?
Hakuna sheria zilizokusudiwa na kutambuliwa kwa wanaobeba mimba kwa niaba, kwahiyo wazazi wengi na watoto hubaki wakihaha na wengine hubaki bila utaifa.

Huchukua miezi chungu nzima kumrejesha mtoto aliyetokana na mama aliyebeba mimba kwa niaba, nyumbani kwao kwa asili, kwani huwa hawatambuliki moja kwa moja kama wazazi wao halali.

"Huko Thailand, mama wanaobeba mimba kwa niaba, wanaonekana kuwa mama halali, kwahiyo iwapo wazazi watamwacha mtoto na mama, basi yeye kisheria ana haki,” anasema Bi Scott.

"Huko India, wazazi waliokusudiwa kukabidhiwa mtoto huonekana kuwa wazazi halali, ambapo kutokana na sheria ya Uingereza, mama aliyebeba mimba kwa niaba, anatambulika kama mama halali.

“Hii inamaanisha mtoto aliyezaliwa na mama aliyebeba mimba kwa niaba nchini India, kutokana na wazazi wa Uingereza, amezaliwa bila utaifa, na lazima aombe uraia wa Uingereza.”


Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

Monday 15 December 2014

USO UNAPOKUWA 'SIVYO NDIVYO'



Woman recovering from plastic surgery, from the series Beauty Recovery Room

Huwezi kukwepo matangazo. Kila pahala unapopita mjini Seoul unashauriwa kubadili umbile lako kwa njia ya upasuaji.

Gangnam eneo lenye utajiri, kila ukuta unaonyesha kuwa na alama ikiashiria upasuaji

Kwenye treni na barabarani, unaambiwa unaweza “kuupa uso wako uhai”. “upasuaji wa matiti”, “kukupa ujana”. Pia kuna “kupunguza taya” (matangazo hayo hasa kwa wanaume).

Mmoja alilalalamika kwamba kidevu chake huuma wakati wa mvua. Halafu baadae ikajulikana alikwenda kufanyiwa upasuaji wa pua lakini akashawishiwa- au akajishawsihi mwenyewe – kuwa kidevu chake kilihitaji kubadilishwa.

Matokeo yake akapata kidevu alichotaka lakini chenye maumivu zaidi. Licha ya yote hayo, bado ana nia ya kuongeza ukubwa wa matiti yake.

Kim Bok-soon spent 30 million won (£17,320) for 15 surgeries on her face over the course of a day and only afterwards found out her doctor was not a plastic surgery specialist
Kim Bok-Soon alishawishiwa kutumia paundi 17,320) kwa upasuaji wa uso mara 15

Korea kusini, wazazi huwapa zawadi mabinti zao vijana, kwa kile wanachoita “upasuaji mara mbili wa kope” unaofanya macho yawake zaidi – “yasiwe macho ya Ki-Asia”. Sababu haieleweki , wakati macho ya WaKorea yanaonekana mazuri jinsi yalivyo.

Jibu linalotokana na matangazo kwenye treni ni kwamba “kujiamini kwa umbo lako kunasababisha kuwa na imani chanya ambapo huweza kuwa msingi wa furaha”. Furaha- inayopatikana kirahisi kwa upasuaji!

Isipokuwa sasa, bila shaka, sivyo inavyoaminiwa. Hali imegeuka, mfululizo wa kesi mahakamani ambapo wagonjwa au waathirika kama wanavyojulikana- wanawashtaki madaktari waliobadilisha sura zao, lakini si kwa uzuri.

Muathrika mmoja alisema ‘bandage’ zilipotolewa: “Huu si uso wa binadamu. Unatisha hata kuliko jini au watu wa sayari nyingine.”

                                                                                                                      

Sunday 14 December 2014

TAALUMA 10 ZINAZOONGOZA KUNYWA KAHAWA



coffee cup

Kikombe cha kahawa asubuhi ni kinywaji ambacho wengi wetu huanza nacho.

Kama unahisi bila hiyo huwezi kuanza siku yako vizuri, basi ujue si peke yako.

Miongoni mwa wanataaluma 10,000 walioshiriki kwenye utafiti ulioafanywa na Pressat, asilimia 85 walisema wanakunywa takriban vikombe vitatu vya kahawa kwa siku.

Na takriban asilimia 70 walikiri kuwa ufanyaji wao wa kazi utaathirika bila kupata kikombe cha kahawa.

Inaonekana kunywa kahawa ni jambo la lazima kazini kwa wataalamu wengi. Wanaokunywa zaidi, hadi vikombe vinne kwa siku, ni wenye kazi zenye mikiki zaidi ‘stress’: waandishi wa habari ndio wanaokunywa kahawa, wakifuatiwa na maafisa polisi na walimu.

Utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Chuo Kikuu cha South Carolina kimegundua kuwa   mtu asizidishe milligram 200 za caffeine kwa siku, ambazo ni sawa na vikombe vinne vya kahawa.

Kunywa kahawa kwa wingi ili tu kuweza kupambana na tafrani na uchovu wa kazi unaweza kusababisha hatari kwa afya yako, kuanzia kupooza na wasiwasi, na hadi kupata matatizo ya moyo, japo utafiti huo umeonyesha asilimia 62 ya wafanyakazi hawakujua athari za kiafya zinazowakabili.

Kwa wastani utafiti huo umeonyesha kuwa wanaume wanakunywa kahawa zaidi kuliko wanawake lakini zaidi kidogo kwa asilimia 5.

Zifuatazo ni taaluma kumi zinazokunywa sana kahawa, kulingana na utafiti:

  • Waandishi wa habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari
  • Maafisa wa polisi
  • Walimu
  • Mafundi bomba
  • Wauguzi na wafanyakazi wa afya
  • Wakurugenzi wa kampuni
  • Wauzaji bidhaa kwa njia ya simu
  • Watoa huduma za IT
  • Wafanyakazi wa maduka ya rejareja
  • Madereva  

 Chanzo: pressat.co.uk
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu



Tuesday 9 December 2014

VIFO KUTOKANA NA MALARIA VYAPUNGUA KWA NUSU



Mosquito

Jitihada za dunia zimepunguza nusu ya watu wanaokufa na malaria – ambapo ni mafanikio makubwa, kulingana na Shirika la Afya Duniani WHO.

Linasema kati ya mwaka 2001 na 2003, vifo milioni 4.3 vimezuiwa, ambapo milioni 3.9 miongoni mwao ni watoto walio chini ya umri wa miaka mitano eneo la kusini mwa jangwa la Sahara.

Kila mwaka, watu wengi zaidi wanapata dawa za kuwakinga na malaria, WHO limesema.

Mwaka 2004, 3% walio hatarini kupata ugonjwa huo walikuwa na uwezekano wa kupata chandarua, lakini sasa ni 50%.

Kushinda mapambano

Idadi ya watu wanaopima imeongezeka, na watu wengi zaidi wana uwezo wa kupata dawa kutibu vijidudu vya malaria, inayosambazwa na kung’atwa na mbu mwenye vidudu hivyo.

Nchi nyingi sasa zinaelekea kuutokomeza kabisa ugonjwa huo.


child sleeping under a bed net

Mwaka 2013, nchi mbili - Azerbaijan na Sri Lanka – waliripoti kutokuwepo na mgonjwa hata mmoja wa maradhi hayo kwa mara ya kwanza, na nyingine 11 (Argentina, Armenia, Misri, Georgia, Iraq, Kyrgyzstan, Morocco, Oman, Paraguay, Turkmenistan na Uzbekistan) nao wamefanikiwa kutokuwa na kesi mpya.  

Barani Afrika, ambapo 90% ya vifo vyote vya malaria hutokea hapo, imepungua kwa kiwango kikubwa.

Idadi ya watu waliopata maradhi hayo barani humo imepungua kwa robo – kutoka watu milioni 173 mwaka 2000 hadi milioni 128 mwaka 2013.

Hii ni licha ya ongezeko la 43% ya idadi ya watu barani Afrika wanaoishi maeneo yaliyo rahisi kupata maradhi hayo.

Sunday 7 December 2014

MARAIS MATAJIRI WA BARA LA AFRIKA 2014

   

Afrika ni bara la pili kwa ukubwa duniani. Pia ni bara la pili lenye watu wengi sana na linachukuliwa kuwa bara maskini mno.

Kuna mataifa 47 ya Afrika yanayoongozwa na viongozi walioongoza kwa zaidi ya muongo mmoja.

Baadhi ya viongozi hawa na familia zao ni matajiri sana na mali zao zinaonekana kupatikana isivyo halali. Wanapata mali zao kutoka maliasili za mataifa hayo.

Marais na Wafalme 8 matajiri wa Afrika wa mwaka 2014. Bonyeza hapa: http://bit.ly/1BqRbn9