Wednesday 3 June 2020

Naibu gavana wa jimbo la Bauchi, Nigeria apatwa na Covid-19


Baba Tela, the Deputy Governor of Bauchi State
Baba Tela, Naibu gavana wa jimbo la Bauchi

Naibu gavana wa jimbo lililopo kaskazini- magharibi mwa jimbo la Bauchi amepima na kukutwa na maambukizi ya virusi vya corona.

Afisa wa shirika la habari alisema Baba Tela amejitenga kwa sasa na watu wote waliomkaribia wakati hao wamechukuliwa vipimo vyao.

Inadhaniwa kuwa naibu gavana huyo aliambukizwa virusi hivyo wakati akifanya kazi kama mwenyekiti wa kikosi kazi kinachosimamia masuala ya virusi vya korona, kulingana na taarifa iliyotolewa na serikali.

Alishaonyesha dalili ya kuambukizwa virusi hivyo kabla ya kuchukuliwa vipimo hivyo.

Jimbo hilo limethibitishwa kuwa na watu 241 wenye maambukizi ya virusi hivyo kati ya takriban watu 10,000 walioambukizwa nchini humo.

Chanzo: BBC

No comments:

Post a Comment