Tuesday 2 June 2020

Hofu ya maambukizi yasimamisha shule kufunguliwa Uganda


Serikali itaendelea na mpango wake wa kusambaza chakula cha msaada


Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameahirisha hatua ya kufungua shule upya kwa wanaomaliza mwaka wao wa mwisho. Amesogeza muda kwa mwezi mmoja zaidi.

Kiongozi huyo alisema kufungua shule upya ni hatari kwani nchi hiyo haina vifaa vya kupimia wanafunzi kila baada ya wiki mbili.

Rais Museveni alisema televisheni mbili zitagaiwa katika kila kijiji kuruhusu wanafunzi kuendelea kujifunza kupitia masomo yanayotolewa kwenye televisheni.

Wakati huo huo, bodaboda bado haziruhusiwi kubeba abiria lakini zinaweza kusafirisha bidhaa.

Makanisa, misikiti, baa, majumba ya starehe na sehemu za kufanyia mazoezi zitaendelea kufungwa kwa siku nyingine 21.

Maduka yameruhusiwa kufunguliwa ilimradi tu yahakikishe wateja wanakaa umbali wa mita 2 kila mmoja.

Kwa taarifa zaidi bonyeza link ifuatayo https://bbc.in/2MrNisl

No comments:

Post a Comment