Showing posts with label Siasa. Show all posts
Showing posts with label Siasa. Show all posts

Tuesday 9 June 2020

Kiongozi wa upinzani Tanzania atarajiwa kupelekwa Dar


Kiongozi wa Chadema Freeman Mbowe (katikati) anaendelea na matibabu hospitali

Kiongozi wa upinzani Tanzania, Freeman Mbowe ameshambuliwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana kwenye mji mkuu Dodoma.

Msemaji wa chama chake cha Chadema amethibitisha tukio hilo kwa Idhaa ya Kiswahili ya BBC.

Amesema kiongozi huyo wa chama alikuwa akirejea nyumbani kwake siku ya Jumatatu washambuliaji walipomvamia na kumjeruhi mguu.

Mnadhimu mkuu wa upinzani Ester Bulaya alisema kuna mipango inafanyika kumsafirisha Mbowe kwa njia ya anga na kumpeleka jijini Dar es Salaam kwa matibabu zaidi kutokana na shambulio hilo.

Viongozi mbalimbali wamemtembelea kiongozi huyo hospitalini akiwemo Naibu Spika, Dr.Tulia Ackson na Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai.

Kulingana na mbunge wa Iringa mjini Peter Msigwa, alikuwepo nyumbani kwa mwenyekiti huyo jana jioni pamoja na Godbless Lema, Joseph Mbilinyi na John Heche.

Chanzo: BBC na https://bit.ly/3cOuOx7

Thursday 2 April 2015

KATIBA MPYA TZ: HAKUNA KURA YA MAONI APRILI 30

Mwenyekiti wa Nec Jaji Mstaafu Damian Lubuva

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) imekubali kuahirisha upigiaji Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa iliyopangwa kufanyika Aprili 30, mwaka huu kutokana na kutokamilika kwa uandikishaji wa Daftrai la kudumu la wapiga kura kwa kutumia teknolojia ya Biometric Voters Registration (BVR).

Hatua hiyo inakuja baada ya kuwepo mfululizo wa matamko na ushauri kutoka kwa wadau mbalimbali wa demokrasia kwamba zoezi hilo lisingewezekana kwa sasa hasa kutokana kusuasua kwa mwenendo wa BVR.

Mwenyekiti wa Nec Jaji Mstaafu Damian Lubuva aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuwa kazi ya uboreshaji daftari la wapiga kura ni ya msingi kabla ya taratibu zote za upigaji kura.

Jaji Lubuva aliyeonekana kuwa mpole zaidi, alisema kwa uzoefu walioupata Njombe, zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura bado halijakamilika katika mkoa huo na mingine iliyosalia.

“Hivyo tume haitaweza kuendelea na zoezi la upigaji kura ya maoni na zoezi hilo lililotangazwa hapo awali kufanyika Aprili 30, 2015 limeahirishwa hadi tarehe itakapotangazwa na Nec baada ya kushauriana na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar,” alisema Jaji Lubuva.

Kwa nyakati tofauti, vyama vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za kidini na wananchi wamekuwa wakiishauri Nec kuahirisha Kura ya Maoni huku vyama vya siasa vikimtaka Rais Jakaya Kikwete atii makubaliano yaliyofikiwa na Kituo cha Demokrasia (TCD) mwaka jana ya kuahirisha zoezi hilo hadi baada ya Uchaguzi mkuu.

Jaji Lubuva alisema kuwa tume yake inaendelea kuboresha daftari la wapiga kura nchi nzima ambapo wanatarajia kukamilisha ifikapo Julai mwaka huu. Nec ilieleza kuwa baada ya kumaliza uandikishaji mkoani Njombe watahamia mikoa ya Ruvuma, Lindi, Mtwara na Iringa.

Chanzo: mwananchi.co.tz

Tuesday 31 March 2015

MUHAMMADU BUHARI ASHINDA NIGERIA



File photo: Goodluck Jonathan (left) and Muhammadu Buhari shake hands after signing a peace deal agreeing to respect the outcome of the polls
Goodluck Jonathan (kushoto) na Muhammadu Buhari walikubaliana wiki iliyopita kuheshimu matokeo ya uchaguzi

Aliyekuwa kiongozi wa kijeshi Muhammadu Buhari amekuwa mgombea wa kwanza wa upinzani kushinda uchaguzi wa urais Nigeria.

Chama cha Jenerali Buhari kimesema mpinzani wake, Goodluck Jonathan, alikubali kushindwa na kumpa pongezi.

Bw Jonathan alipishana na Jenerali Buhari kwa takriban kura milioni mbili alipogoma mara ya kwanza kukubali kushindwa.

Waangalizi kwa ujumla wameusifia uchaguzi lakini kumekuwa na madai ya udanganayifu, ambao baadhi wanahofia kunaweza kusababisha maandamano na ghasia.

Kwa taarifa zaidi, bonyeza link ifuatayo

http://www.bbc.co.uk/news/world-africa-32139858

BUHARI 'ANAONEKANA' KUONGOZA UCHAGUZI NIGERIA



People watch election news coverage on television at a street in Lagos, Nigeria, 30 March 2015

Matokeo ambayo bado hayajakamilika kutoka uchaguzi wa Nigeria unaashiria aliyekuwa kiongozi wa kijeshi Muhammadu Buhari amepata kura zaidi kuliko rais wa sasa aliye madarakani, Goodluck Jonathan.

Hata hivyo, majimbo yenye watu wengi zaidi kama vile Lagos na Rivers bado matokeo hayakutangazwa rasmi.

Huku nusu tu ya majimbo ya Nigeria yakiwa yametangazwa, chama cha Jenerali Buhari cha All Progressives Congress (APC) kiliripotiwa kuwa na kura zaidi kwa milioni mbili.

Matokeo zaidi yanatarajiwa kutangazwa siku ya Jumanne.

Tume ya uchaguzi ya Nigeria (Inec) ilisitisha kutangaza matokeo Jumatatu usiku, baada ya kutoa matokeo ya majimbo 18 na mji mkuu Abuja.

Chama cha Rais Jonathan cha People's Democratic Party (PDP) kilipata kura 6,488,210 na cha APC cha Jenerali Buhari kimepata kura 8,520,436.

                                                                                                                                                                                        

Monday 30 March 2015

UCHAGUZI NIGERIA: MATOKEO YA AWALI YATARAJIWA



An official of the Independent National Electoral Commission retrieves on March 29, 2015 documents from ballot boxes from the presidential election

Tume ya kusimamia uchaguzi Nigeria imesema inatarajia kutangaza matokeo ya awali ya uchaguzi wa Rais siku ya Jumanne baada ya raia wa nchi hiyo kupiga kura Jumamosi.

Rais aliye madarakani Goodluck Jonathan anakabiliwa na changamoto nzito kutoka kwa aliyekuwa kiongozi wa kijeshi Muhammadu Buhari.

Umoja wa mataifa umeusifia upigaji kura huo licha ya kuwepo hitilafu za kiufundi, maandamano na ghasia yanayohusishwa na Boko Haram

Upigaji kura uliendelea mpaka siku ya pili katika baadhi ya sehemu nchini Nigeria baada ya kuwepo matatizo ya mfumo mpya wa kutumia kadi za kielektroniki.

 

Wednesday 25 March 2015

ALIYEKUWA RAIS WA LIBERIA KUFUNGWA UINGEREZA



 Charles Taylor in court (file photo)

Imetolewa amri kuwa aliyekuwa rais wa Liberia Charles atatumikia kipindi chake chote cha gerezani Uingereza, baada ya kukataliwa kuhamishiwa Rwanda.

Alisema ananyimwa haki yake ya maisha na familia yake, kwasababu mke wake na watoto wake wamenyimwa viza ya Uingereza.

Majaji walikana kauli yake hiyo, wakisema hawakuomba viza hiyo inavyotakiwa.

Mahakama inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ilimtia hatiani juu ya uhalifu wa kivita kwa kuwaunga mkono waasi waliofanya ukatili Sierra Leone.


Tuesday 17 March 2015

WABUNGE WA UPINZANI 21 WAFUKUZWA ZIMBABWE


 Morgan Tsvangirai greeting supporters in Harare in 2014
Wabunge wa upinzani 21 wamefukuzwa kutoka bunge la Zimbabwe baada ya kujitoa na kuunda chama kipya.

Spika Jacob Mudenda aliagiza kufukuzwa kwa wabunge hao, wanaoongozwa na aliyekuwa waziri wa fedha Tendai Biti.

Kundi hilo liligombea uchaguzi wa mwaka 2013 chini ya Morgan Tsvangirai wa chama cha Movement for Democratic Change (MDC).

Baadae wakagawanyika kuunda MDC mpya baada ya kukataa uongozi wake.

Kufukuzwa kunatoa fursa kwa uchaguzi mdogo kwenye majimbo ya wabunge hao 14 ambao walichaguliwa moja kwa moja, aliripoti mwandishi wa habari wa BBC Brian Hungwe kutoka kutoka mji mkuu Harare.