Monday 30 March 2015

UCHAGUZI NIGERIA: MATOKEO YA AWALI YATARAJIWA



An official of the Independent National Electoral Commission retrieves on March 29, 2015 documents from ballot boxes from the presidential election

Tume ya kusimamia uchaguzi Nigeria imesema inatarajia kutangaza matokeo ya awali ya uchaguzi wa Rais siku ya Jumanne baada ya raia wa nchi hiyo kupiga kura Jumamosi.

Rais aliye madarakani Goodluck Jonathan anakabiliwa na changamoto nzito kutoka kwa aliyekuwa kiongozi wa kijeshi Muhammadu Buhari.

Umoja wa mataifa umeusifia upigaji kura huo licha ya kuwepo hitilafu za kiufundi, maandamano na ghasia yanayohusishwa na Boko Haram

Upigaji kura uliendelea mpaka siku ya pili katika baadhi ya sehemu nchini Nigeria baada ya kuwepo matatizo ya mfumo mpya wa kutumia kadi za kielektroniki.

 

No comments:

Post a Comment