Monday 2 March 2015

MWANASIASA MAARUFU BURUNDI ATOROKA JELA













Mmoja wa wanasiasa maarufu wa upinzani nchini Burundi, Hussein Radjabu ametoroka gerezani.

Ametoroka na wafungwa wengine watatu na polisi wanne wenye silaha, akiwemo mkuu wa usalama wa gereza hilo.

Haileweki aliwezaje kutoroka.

Bw Radjabu amekuwa akitumikia kifungo cha miaka 13 kwa kupanga njama ya kuipindua serikali.

Kabla ya kukamatwa mwaka 2007, Hussein Radjabu, alikuwa mshirika wa karibu wa Rais Pierre Nkurunziza na Mwenyekiti wa Chama Tawala.

Haya yanatokea wakati kuna hali ya wasiwasi wa kisiasa nchini Burundi kabla ya uchaguzi unaotarajia kufanyika baadae mwaka huu.

No comments:

Post a Comment