Monday 23 March 2015

KENYA YAMWACHIA HURU BIBI WA MIAKA 100



Nairobi skyline

Bibi wa miaka 100 ameachiliwa huru kutoka gereza moja nchini Kenya baada ya kufanyika kampeni ya kitaifa ya kutaka aachiwe.

Margaret Ngima alifungwa katika gereza la Embu wiki iliyopita kwa kutoheshimu mahakama baada ya kushindwa kulipa faini ya dola elfu moja.

Bibi huyo wa mabibi alishutumiwa kwa kupuuza amri ya mahakama katika mgogoro wa ardhi na familia nyingine.

Kesi yake ilizusha hasira kali Kenya, na hatimaye faini yake kulipwa na seneta wa Nairobi  Mike Sonko.

No comments:

Post a Comment