Friday 13 March 2015

UPANDIKIZAJI WA KWANZA WA UUME 'KUFANIKIWA'


 Surgical team

Mchakato wa kwanza kufanikiwa duniani wa kupandikiza  uume ‘transplant’ umeripotiwa kufanyika Afrika kusini.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 21, ambaye hatotambulishwa hadharani, alipoteza uume wake wakati wa mchakato wa kutahiriwa kufanyika vibaya.

Madaktari mjini Cape Town walisema upasuaji huo ulifanikiwa na mgonjwa alikuwa na furaha na afya njema.

Kundi hilo la madaktari lilisema kulikuwa na mjadala mzito wa kujadili iwapo upasuaji huo, ambao si suala la kuokoa maisha kama ilivyo kwa upasuaji wa kupandikiza moyo, ulifuata maadili ya tiba.

Kumewahi kuwa na jaribio kama hilo, moja ikiwa China. Inasadikiwa kuwa upasuaji ulifanikiwa, lakini baadae uume huo haukufanya kazi.

Kubadilishiwa uume

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 18 tayari alikuwa na uzoefu wa mapenzi alipotahiriwa.

Mchakato huo ni sehemu ya kukua kutoka utoto kuingia ujana katika baadhi ya sehemu za Afrika kusini.

Man from Xhosa tribe
Sherehe za jando Afrika kusini
Alibaki na sentimeta moja tu ya uume wake halisi baada ya kutahiriwa.

Madaktari Afrika kusini walisema wana watu wengi wanaohitaji kupandikizwa uume duniani kote.

Wengi, japo wengine husema mamia, ya vijana wa kiume hufariki dunia kila mwaka wakati wa sherehe za kutahiriwa.

Chanzo: BBC 
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

1 comment: