Wednesday 25 March 2015

ALIYEKUWA RAIS WA LIBERIA KUFUNGWA UINGEREZA



 Charles Taylor in court (file photo)

Imetolewa amri kuwa aliyekuwa rais wa Liberia Charles atatumikia kipindi chake chote cha gerezani Uingereza, baada ya kukataliwa kuhamishiwa Rwanda.

Alisema ananyimwa haki yake ya maisha na familia yake, kwasababu mke wake na watoto wake wamenyimwa viza ya Uingereza.

Majaji walikana kauli yake hiyo, wakisema hawakuomba viza hiyo inavyotakiwa.

Mahakama inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ilimtia hatiani juu ya uhalifu wa kivita kwa kuwaunga mkono waasi waliofanya ukatili Sierra Leone.


No comments:

Post a Comment