Thursday 26 March 2015

MAREKANI YAONYA KUWEPO SHAMBULIO KAMPALA



A crowded street in Kampala. File photo
Marekani yaonya kuwepo shambulio Kampala

Ubalozi wa Marekani nchini Uganda umeonya kuwa raia kutoka nchi za kimagharibi – wakiwemo Wamarekani – huenda wakawa wamelengwa kwa mashambulio ya ugaidi katika mji mkuu Kampala.

Ulisema “umepata taarifa za uwezekano wa kuwepo vitisho” kwenye maeneo ya mijini ambapo aghlabu raia wa kigeni hujikusanya.

Shambulio “huenda likatokea hivi karibuni” ilisema, huku ikisema mikutano mengine iliyokuwa imepangwa kufanyika katika hoteli za Kampala imeahirishwa.

Ubalozi huo haujatoa taarifa zaidi. Uganda imeshawahi kushambuliwa siku za nyuma na wapiganji wa Kisomali wa al-Shabab.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment