Thursday 19 March 2015

MAREKANI YAMWUUA KIONGOZI WA AL-SHABAB



Armed members of the militant group al-Shabab attend a rally on the outskirts of Mogadishu, Somalia in this February 2012 file photo.

Wizara ya ulinzi ya Marekani imethibitisha kumwuua kiongozi wa al-Shabab, Adan Garar.

Pentagon ilisema mpiganaji huyo alipigwa na kombora kaskazini mwa Somalia siku ya Ijumaa.

Garar alikuwa mshukiwa wa shambulio la Westgate mwaka 2013 mjini Nairobi lililosababisha mauaji ya watu 67.  

Marekani iliiamini Garar alikuwa akisimamia harakati “zilizowalenga Marekani na raia wengine wa kigeni”.

Alikuwa mwanachama wa usalama na ujasusi na pia “kiongozi aliyehusika na harakati zote za nje za al-Shabab”, kulingana na Pentagon.

Harakati hizo zilifanyika takriban kilomita 240, magharibi mwa Mogadishu karibu na mji wa Dinsoor.

No comments:

Post a Comment