Friday 27 March 2015

HIV: DHARURA YA KIAFYA KUTANGAZWA INDIANA



Computer artwork of the HIV virus

Gavana wa Indiana ametangaza dharura ya afya ya umma baada ya mlipuko wa HIV “kufikia kiwango cha kusambaa” sehemu ya jimbo hilo.

Kaunti ya Scott, eneo la kimaskini ambapo watumiaji wa dawa za kulevya kutumia sindano moja kwa pamoja si jambo la ajabu, ambapo katika wiki za hivi karibuni maambukizi mapya 79 yameongezeka kutoka wastani wa watu watano.

 Gavana Mike Pence ameidhinisha maafisa wa afya kutekeleza mradi wa kutoa elimu juu ya kubadilishana sindano – jambo alilowahi kukataa siku za nyuma.

HIV ni kirusi kinachosababisha ugonjwa wa Aids.

Mlipuko huo mwanzo ulitambuliwa mwezi Januari mwishoni. Tangu wakati huo, maafisa wamegundua watu 79 wakiwa na ugonjwa huo – kutoka watu 26 tu mwezi uliopita.

No comments:

Post a Comment