Monday 30 March 2015

MWENDESHA MASHTAKA WA UGANDA AUAWA



Security checks in Kampala, 26 March
Ulinzi uliimarishwa baada ya onyo la shambulio la ugaidi

Joan Kagezi, mwendesha mashtaka mkuu wa Uganda katika kesi ya watu 13 walioshutumiwa kwa shambulio kubwa la bomu la al-Shabab, amepigwa risasi na kufariki dunia mjini Kampala.

Bi Kagezi alilengwa na watu wenye silaha waliokuwa kwenye pikipiki alipokuwa njiani akielekea nyumbani.

Shambulio la bomu la kujitoa mhanga la mwaka 2010 Kampala lilisababisha vifo vya watu 76 walipokuwa wakitazama fainali ya Kombe la Dunia.

Wiki iliyopita, ubalozi wa Marekani Uganda iliwaonya raia wote wa kigeni – wakiwemo Wamarekani – uwezekano wa kulengwa na mashambulio ya “kigaidi” mjini Kampala.

Bi Kagezi, wakili mwandamizi, aliongoza idara ya umma ya kuzuia ugaidi na pia idara ya uhalifu wa kivita.

Msemaji wa polisi wa Kampala Patrick Onyango alisema: "Walikuwa wakimfuatilia na pikipiki – walimpiga risasi na kumwuua.


No comments:

Post a Comment