Wednesday 25 March 2015

JEREMY CLARKSON ATOLEWA TOP GEAR YA BBC



Jeremy Clarkson

Mkataba wa Jeremy Clarkson hautoongezwa baada ya kufanya "shambulio lisilokuwa na uchochezi wowote” kwa msimamizi wa kipindi cha Top Gear, mkurugenzi mkuu wa BBC amethibitisha.

Tony Hall alisema “hakuchukua uamuzi huo kwa uwepesi” na alitambua “itagawanya maoni ya wengi”.

Hata hivyo, aliongeza “alivuka mpaka” na " hawezi kukubaliana na kilichofanyika katika tukio hilo".

Clarkson alisimamishwa kazi Machi 10, kwa kile kilichoitwa “ugomvi” na msimamizi wa Top Gear Oisin Tymon.

Ugomvi huo, uliotokea kwenye hoteli moja huko Yorkshire, inasemwa kuwa ilitokea kwasababu hapakuwepo na chakula cha moto baada ya kufanya kazi siku nzima.

No comments:

Post a Comment