Wednesday 25 March 2015

TAKRIBAN WATOTO 500 HAWAJULIKANI WALIPO



Boko Haram leader Abubakar Shekau (12 May 2014)

Takriban watoto 500 wenye umri wa miaka 11 na chini ya hapo hawajulikani walipo katika mji mmoja Nigeria uliotekwa upya na wapiganaji, aliyekuwa mkazi wa Damasak aliiambia BBC.

Mfanyabiashara mmoja wa mji huo ulio kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa Boko Haram waliwachukua watoto hao walipokimbia.

Majeshi kutoka Niger na Chad waliuteka mji wa Damasak mapema mwezi Machi, na kuzima udhibiti wa mji huo kwa miezi kadhaa na wapiganaji hao.

Jesho la eneo hilo hivi karibuni limekuwa likiisaidia Nigeria kupambana na wapiganaji hao.

Maelfu wameuawa tangu mwaka 2009, wakati Boko Haram ilipoanza mapigano kwa nia ya kuunda taifa la Kiislamu.

No comments:

Post a Comment