Monday 1 June 2020

VIRUSI VYA CORONA: SHULE ZAFUNGULIWA ENGLAND ILA WAZAZI BADO WANA MASHAKA


first day back at school
Wazazi wakirejesha watoto wao shuleni huko Norfolk, leo Jumatatu



Wanafunzi wa shule za msingi katika baadhi ya shule England wanarejea- lakini utafiti waonyesha nusu ya wazazi huenda wamewabakiza watoto wao nyumbani.

Kuna hisia tofauti kufuatia shule hizo kufunguliwa upya, hata hivyo katika baadhi ya maeneo shule zitaendela kufungwa.

Watoto kutoka darasa la kwanza hadi la 6 ndio wanaoweza kurejea shuleni, wengi wao ambao hawakwenda darasani kwa wiki 10.

Hatua hii inachukuliwa huku masharti ya kujifungia ndani ‘lockdown’ yakilegezwa, ikiwemo ruhusa ya watu sita kwa pamoja kuweza kukutana katika mazingira ya nje.

Kwa maelezo zaidi bonyeza link ifuatayo https://bbc.in/3cmtfpR




No comments:

Post a Comment