Monday 15 December 2014

USO UNAPOKUWA 'SIVYO NDIVYO'



Woman recovering from plastic surgery, from the series Beauty Recovery Room

Huwezi kukwepo matangazo. Kila pahala unapopita mjini Seoul unashauriwa kubadili umbile lako kwa njia ya upasuaji.

Gangnam eneo lenye utajiri, kila ukuta unaonyesha kuwa na alama ikiashiria upasuaji

Kwenye treni na barabarani, unaambiwa unaweza “kuupa uso wako uhai”. “upasuaji wa matiti”, “kukupa ujana”. Pia kuna “kupunguza taya” (matangazo hayo hasa kwa wanaume).

Mmoja alilalalamika kwamba kidevu chake huuma wakati wa mvua. Halafu baadae ikajulikana alikwenda kufanyiwa upasuaji wa pua lakini akashawishiwa- au akajishawsihi mwenyewe – kuwa kidevu chake kilihitaji kubadilishwa.

Matokeo yake akapata kidevu alichotaka lakini chenye maumivu zaidi. Licha ya yote hayo, bado ana nia ya kuongeza ukubwa wa matiti yake.

Kim Bok-soon spent 30 million won (£17,320) for 15 surgeries on her face over the course of a day and only afterwards found out her doctor was not a plastic surgery specialist
Kim Bok-Soon alishawishiwa kutumia paundi 17,320) kwa upasuaji wa uso mara 15

Korea kusini, wazazi huwapa zawadi mabinti zao vijana, kwa kile wanachoita “upasuaji mara mbili wa kope” unaofanya macho yawake zaidi – “yasiwe macho ya Ki-Asia”. Sababu haieleweki , wakati macho ya WaKorea yanaonekana mazuri jinsi yalivyo.

Jibu linalotokana na matangazo kwenye treni ni kwamba “kujiamini kwa umbo lako kunasababisha kuwa na imani chanya ambapo huweza kuwa msingi wa furaha”. Furaha- inayopatikana kirahisi kwa upasuaji!

Isipokuwa sasa, bila shaka, sivyo inavyoaminiwa. Hali imegeuka, mfululizo wa kesi mahakamani ambapo wagonjwa au waathirika kama wanavyojulikana- wanawashtaki madaktari waliobadilisha sura zao, lakini si kwa uzuri.

Muathrika mmoja alisema ‘bandage’ zilipotolewa: “Huu si uso wa binadamu. Unatisha hata kuliko jini au watu wa sayari nyingine.”

                                                                                                                      

No comments:

Post a Comment