Wednesday 17 December 2014

SHERIA ZA WATOTO 'KUTOKA WATU WATATU'


Babies

Sheria ya kutengeneza watoto kutoka watu watatu – ambapo inasemwa wawili tu watakuwa wazazi halali- imetangazwa na serikali ya Uingereza.

Mbinu hiyo ya uzalishaji itatumia nasaba kutoka kwa mama, baba na mwanamke wa kujitolea ili kuzuia maradhi.

Wabunge hivi karibuni watapiga kura ili kuifanya Uingereza nchi ya kwanza duniani kuhalalisha utaratibu huo au la.

Wapinzani wanasema ni kinyume cha maadili kutengeneza watoto kutumia asidi nasaba, DNA kutoka watu watatu.

Wanasayansi wa Uingereza walioongoza utafiti huo wanatarajia kuanza kutumia utaratibu huo mwakani.

No comments:

Post a Comment