Wednesday 24 December 2014

GEORGE HW BUSH APELEKWA HOSPITALI



 File photo of George H W Bush, July 2013
Aliyekuwa rais wa Marekani George Bush Senior amepelekwa hospitali baada ya kukosa pumzi, msemaji wake alisema.

Bw Bush, mwenye umri wa miaka 90, alipelekwa hospitali ya Houston Methodist kama kuangaliwa na “atafanyiwa uchunguzi”, pia tena uangalizi tu, alisema Jim McGrath.

Miaka miwili iliyopita, Bw Bush alitibiwa kwenye hospitali hiyohiyo kwa zaidi ya miezi miwili kwa maradhi yanayohusiana na mapafu na kifua na mengineyo.

Alikuwa rais kutoka mwaka 1989 hadi 1993.

Ni rais mzee kuwa hai Marekani na mkongwe miongoni mwa wapiganaji wa Vita Kuu vya Kwanza Vya Dunia.

Kwa sasa hawezi tena kutumia miguu yake. Mtoto wake wa kiume George W Bush alikuwa rais kuanzia mwaka 2001 hadi 2009.

No comments:

Post a Comment