Wednesday 3 December 2014

'MARUFUKU' KUTUMIA JINA SAWA NA LA RAIS


This undated picture released from North Korea's official Korean Central News Agency (KCNA) on January 12, 2014 shows North Korean leader Kim Jong-Un

Korea Kaskazini inaripotiwa kuamuru mtu yeyote mwenye jina sawa na la kiongozi wake Kim Jong-un, kubadili mara moja., kulingana na vyombo vya habari vya Korea kusini.

Taarifa kutoka vyombo vya habari vya Korea Kusini zinasema jina hilo limezuiliwa kupewa  kwa watoto wanaozaliwa kuanzia sasa.

Mbali na hilo na wale wanaolitumia, tayari wanalazimika kubadili vyeti vyao vya kuzaliwa na nyaraka za makazi yao.

Amri hiyo ilitolewa tangu mwaka 2011 lakini ndio kwanza sasa imetolewa hadharani.

Karibu asilimia ishirini ya familia za Kikorea zina jina la Kim na Jong-un.

Japo maelekzo yamenukuliwa kuwa  hatua hiyo ni hiari, waandishi walisema wachache Korea Kaskazini wataacha kutii.

No comments:

Post a Comment