Sunday 21 December 2014

MUHAMMAD ALI APELEKWA HOSPITALI



Muhammad Ali, pictured at a celebrity boxing match in 2012
Ali, aliyepigwa picha hii mwaka 2012, amekuwa na maradhi ya kutetemeka 'Parkinsons' kwa miaka 30 

Aliyekuwa bingwa mara tatu wa uzani wa juu wa masumbwi amepelekwa hospitali akiumwa mapafu ‘pneumonia’, msemaji wake alisema.

Ali, ambaye ana maradhi ya kutetemeka ‘Parkinson’, yuko katika hali nzuri, Bob Gunnell ameviambia vyombo vya habari.

"Uchunguzi unaonekana kuwa mzuri," Bw Gunnell alisema, akiongeza kuwa kukaa kwa mwanandondi huyo mwenye umri wa miaka 72 hospitalini kutakuwa kwa muda mfupi.

Hakutoa taarifa nyingine ya ziada na kutaka ombli la familia ya Ali kuachwa bila kubughudhiwa iheshimiwe.

Ali alipatikana na ugonjwa huo wa kutetemeka mwaka 1984, miaka mitatu baada ya kustaafu ndondi.

Alionekana hadharani katika sherehe mwezi Septemba, eneo alipokuzwa huko Louisville kwa ajili ya Tuzo za kusaidia Binadamu za Muhammad Ali.

No comments:

Post a Comment