Saturday 20 December 2014

MTANZANIA AFUNGWA MAISHA KWA KUUA BINTI ZAKE



Indianna, miaka 3 na Savannah miaka 4




Mtanzania mmoja mwenye uraia wa Australia amefungwa maisha kwa kuua mabinti zake wawili muda mfupi baada ya kuwavalisha magauni na kuwarekodi wakicheza.

Mauaji hayo yanasadikiwa kuchochewa na chuki dhidi ya aliyekuwa mke wake, Jaji alisema.

Charles Amon Mihayo, mwenye umri wa miaka 36, lazima atumikie angalau miaka 31 jela kwa mauaji hayo.

Charles akiwasili mahakamani, mwezi Septemba



Aliwaua binti zake Savannah mwenye umri wa miaka minne na Indianna miaka mitatu kwa kuwaziba pumzi akitumia mto wakati wakicheza kombolea siku ya Jumapili Kuu,.

Mihayo baadae aliwaambia polisi ilibidi lazima afanye mauaji hayo lakini akasema hahitaji kuwapa sababu ya kwanini alifanya hivyo.

Lakini hakimu wa mahakama kuu Lex Lasry alisema uhalifu wake ulifanyika kutokana na mgogoro uliokuwa ukiendelea na aliyekuwa mkewe.

No comments:

Post a Comment