Wednesday 3 December 2014

KESI INAYOMKABILI RAIS KENYATTA ITAENDELEA?


Kenya's President Uhuru Kenyatta leaves after attending the Mashujaa Day (Hero's Day) celebrations at the Nyayo National Stadium in Nairobi, on 20 October 2014.
Bw Kenyatta alichaguliwa mwaka 2013, licha ya kukabiliwa na mashtaka ICC

Mahakama ya uhalifu wa kivita ICC imempa kiongozi wa mashtaka katika mahakama hiyo Fatou Bensouda muda wa wiki moja aondoe mashtaka dhidi ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Kama si hivyo ametakiwa awasilishe taarifa kuelezea ikiwa ana ushahidi wa kutosha kuendeleza kesi hiyo.
Mahakama hiyo imekataa ombi la kiongozi huyo wa mashtaka kuiahirisha kesi dhidi ya Bwana Kenyatta ili kumpa muda kutafuta ushahidi zaidi. 

Bw Kenyatta alikuwa kiongozi wa kwanza wa nchi kufikishwa rasmi mahakamani tangu kushtakiwa mwaka 2012 kwa uhalifu dhidi ya binadamu, jambo analokataa.

Upande wa mashtaka mara kwa mara umeomba muda zaidi kujenga hoja ya kesi hiyo.
Wamesema mashahidi wamekuwa wakihongwa na kutishwa, na serikali ya Kenya imekataa kukabidhi nyaraka muhimu zinazotakiwa.

Bw Kenyatta amekana kuchochea ghasia kufuatia uchaguzi wenye utata mwaka 2007 ili kuzuia ushindi wa kwa wakati ule Rais Mwai Kibaki na kusema kesi ya ICC ni ya kisiasa.

No comments:

Post a Comment