Tuesday 2 December 2014

HIV 'YAPUNGUA MAKALI'



HIV

Virusi vya HIV vinaanza kupungua makali, kulingana na utafiti mkubwa wa kisayansi.

Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford kinaonyesha virusi hivyo “vinafubazwa” huku vikiendana na mfumo wa kinga wa miili yetu.

Utafiti huo unasema maambukizi ya HIV yanachukua muda mrefu zaidi kusababisha Ukimwi na mabadiliko ya virusi huenda ikasaidia jitihada za kuzuia kusambaa kwa maradhi hayo.

Baadhi ya wataalamu wa virusi wanapendekeza virusi hivyo mwisho “vitakuwa havina athari yoyote” kwa jinsi vinavyoendelea kuwepo.

Zaid ya watu milioni 35 duniani wameathirika na virusi vya HIV na ndani ya miili yao mapambano makali huwepo baina ya mfumo wa kinga na virusi hivyo.

No comments:

Post a Comment