Wednesday 31 December 2014

RAIS KENYATTA ATEUA INSPEKTA MPYA WA POLISI

 


Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, amemteua Joseph Kipchirchir Boinet, kuwa Inspekta Jenerali mpya wa polisi nchini humo.

Amechukua nafasi ya , David Kimaiyo, aliyejiuzulu, kufuatia mauaji ya wachimba migodi 36 Mandera, kaskazini-mashariki mwa Kenya.

Boinet alijiunga na shirika la kijasusi mwaka 1998.

Bunge linatarajiwa kuidhinisha uteuzi wake kabla ya kupitishwa rasmi.




No comments:

Post a Comment