Sunday 21 December 2014

UCHUMI WA ZIMBABWE WAZIDI KUSUASUA



A poster showing the new 25 cent bond coin in Zimbabwe

Sarafu maalum zilizotolewa na benki kuu ya Zimbabwe zimesambazwa huku sherehe za Krismas zikikaribia.

Zimbabwe iliacha kutumia sarafu zake mwaka 2009 kutokana na kupanda sana kwa gharama za maisha na mara nyingi hutumia dola za kimarekani na randi za Afrika Kusini.

Lakini kutokana na sarafu hizi kuwa chache, wauza maduka hupewa ‘chenji’ kwa pipi au kalamu.

Gavana wa benki kuu alisema kulikuwa hakuna mpango wa kurejesha upya matumizi ya dola za Zimbabwe na sarafu hizi mpya zitaambatana na dola za kimarekani.


 A Zimbabwean looks at a Z$50bn note issued by Zimbabwe's central bank on 13 January 2009

John Mangudya alisema sarafu zenye thamani ya dola milioni 10 – kwa senti moja, senti 5, senti 10 na senti 25 – mpaka sasa zimesambazwa kwenye mabenki.

Alisema jumla ya fedha zilizosambazwa haitozidi dola milioni 50, kulingana na gazeti la taifa la Zimbabwe, Herlad.

No comments:

Post a Comment