
Wanawake wawili kutoka Saudi Arabia waliotiwa kizuizini kwa kukiuka amri ya kupigwa marufuku kwa madereva wanawake, sasa kesi yao itasikilizwa kwenye mahakama ya ugaidi, wanaharakati walisema.
Loujain al-Hathloul, mwenye umri wa miaka 25, na Maysa al-Amoudi, 33, wamekuwa kizuizini kwa takriban mwezi mzima.
Kesi za wanawake hao zinaripotiwa kuhamishwa kutokana na maneno waliyoandika kwenye mitandao ya kijamii – badala ya kuendesha kwao magari, kulingana na wanaharakati.
Saudi Arabia ni nchi pekee duniani kukataza wanawake kuendesha gari duniani.
Wanaume pekee ndio hupewa leseni ya udereva – na wanawake wanaoendesha gari hadharani huwa hatarini kutozwa faini na kukamatwa na polisi.
Wanawake wa Arabuni wamefanya kampeni nyingi – zikiwemo kwenye mitandao ya kijamii – kutaka vizuizi vipunguzwe.
No comments:
Post a Comment