Monday 1 December 2014

NDOA YA WATU WENGI KWA MPIGO YAFUNGWA BRAZIL



Mass wedding in Rio de Janeiro

Takriban wapendanao 2,000 nchini Brazil wameoana katika eneo moja mjini Rio de Janeiro, kwenye harusi kubwa ya watu wengi kwa pamoja iliyoweka historia mjini humo.

Tukio hilo la kila mwaka, linalopigiwa chapuo na mamlaka za eneo hilo, lina nia ya kusaidia wapendanao wenye kipato kidogo wasio na uwezo wa kulipia gharama za harusi.


Mamlaka za Rio zilikodisha treni maalum kwa ajili ya wapendanao hao na wageni wao waalikwa.

Takriban watu 12,000 walihudhuria shughuli hiyo katika uwanja wa Maracanazinho.

Majaji walijitolea kuidhinisha shughuli hiyo.



Mass wedding in Rio de Janeiro
Watarajiwa wenye kipato cha dola 640 kwa mwezi waliruhusiwa kufungishwa ndoa kwenye shughuli hiyo 

Wapendanao hao pia walifungishwa ndoa iliyobarikiwa na askofu wa Kikatoliki na padri pia.

Tukio hilo limepewa jina la Dia do Sim", au "Siku ya Nakubali” yaani “I Do Day".

Wengi walioozeshwa walikuwa wakikaa pamoja kwa muda mrefu.

Bw Moraes amekuwa na Ana Rosangela Azevedo,mwenye umri wa miaka 31, tangu mwaka  2010 na mapema mwaka huu waliamua kuhalalisha mahusiano yao.

No comments:

Post a Comment