Monday 29 December 2014

SOMALIA YAANZA KUTOA BIMA KWA 'MARA YA KWANZA'


 

Biashara ya kwanza ya Bima kwa zaidi ya miaka 20 imeanza kwenye mji mkuu Mogadishu nchini Somalia.

Kampuni hiyo (Somali Takaful and Re-Takaful) inayosema inafuata sharia za Kiislamu itaanza kwa kutoa bima za mota na mizigo ya majini.

Mkurugenzi wa kampuni hiyo Mohamed Jesow alisema watu wengi Mogadishu hawajui hata bima ni nini, kwani nchi hiyo imekuwa uwanja wa vita tangu serikali kuu kuporomoka mwaka 1991.

Alisema wateja watakaolipwa fidia ni wale ambao mali zao ziliharibiwa kwa bomu na mashambulio mengine, ilimradi hawakulengwa wao moja kwa moja.

Ulinzi umeimarika Mogadishu katika miezi ya hivi karibuni, lakini kundi la al-Shabab na wengine mara nyingi hufanya mashambulio.



No comments:

Post a Comment