Tuesday 30 December 2014

FURAHA KUONGEZEKA DUNIANI, AFRIKA KINARA



A handout picture taken by Prince Harry shows Lesothan children posing for a photograph at a herd boy school supported in Mokhotlong, Lesotho (December 2014)
Waliohojiwa Afrika ndio wenye furaha zaidi

Watu wenye furaha inaongezeka duniani, kulingana na utafiti wa mwisho wa mwaka wa watu  64,000 katika nchi 65.

Shirika lililofanya utafiti huo WIN/Gallup liligundua kuwa 70% ya waliohojiwa wameridhika na maisha yao – idadi iliyoongezeka kwa 10% kutoka mwaka jana.

Fiji ndilo taifa lenye furaha zaidi, huku 93% ya wakazi wakiwa na furaha na kuridhika, na Iraq ikiwa la mwisho lenye furaha kwa 31%.

Utafiti huo umeonyesha kuwa Afrika ni bara lenye furaha zaidi, huku 83% ya watu wakisema wana furaha au furaha sana.

Wakati huohuo, Ulaya ya Magharibi ilionekana eneo lenye watu wengi wasio na furaha, huku 11%  wakisema hawana furaha au hawana furaha hata kidogo.

Kwa takwimu za ulimwengu, 53% ya waliohojiwa walihisi mwaka 2015 utakuwa mzuri zaidi kuliko 2014.

Robo tatu ya waliohojiwa Afrika walikuwa na matumaini makubwa ya maisha kuimarika, ikilinganishwa na 26% ya waliopo Ulaya ya Magharibi.

Nigeria ndio nchi yenye hisia chanya kuliko zote, huku Lebanon ikiwa yenye hisia hasi kuliko zote.




No comments:

Post a Comment