Sunday 14 December 2014

WATANZANIA CHINA WAUNDA UMOJA WAO

Wadau wakipozi kwa picha
Mdau Geofrey au Mzee wa Shekeli, Charles na Elvis wakisakata rumba kusherehekea uzinduzi wa Natasa

Viongozi wa NATASA. Kutoka kushoto katibu mkuu Halima Guga, Mwenyekiti Given Massawe, Mratibu wa Elimu Abdulkarim Baksh

Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma kwenye mjii wa Nanchang nchini China wameanzisha umoja wao na jana Jumamosi wameuzindua rasmi umoja huo wenye lengo la kuwasaidia kwa mambo mbalimbali wakiwa kwenye nchi ya kigeni.
 

Jumla ya wanafunzi 54 wa Kitanzania wapo kwenye mjii huo wakiwa wanasoma kwenye vyuo mbalimbali na walikuwa hawana kitu chochote kinachowaweka karibu kama Watanzania na ndio maana wakaanzisha umoja huo.
 

Umoja huo unaojulikana kwa jina la Nanchang, Tanzanian Students Association (NATASA) ulizinduliwa ramsi na mwenyekiti wake Given Massawe ambae alisema kuanzishwa kwa umoja huo lilikuwa ni wazo la muda mrefu na hatimae hivi sasa ndoto imetimia.
 

Massawe alifafanua kuwa kwenye mijii mbalimbali mingine ya nchini China ambako kuna wanafunzi wa Kitanzania nao wanajumuia zao ambazo zinawasaidia hivyo kwa wanafunzi wa Nanchang kuwa na umoja huo ni sehemu ya kufungua milango kwao.
 

Mwenyekiti huyo amesema hivi sasa wapo kwenye harakati ya kutengeneza katiba yao ambayo ndio itakuwa dira ya uongozi wao na pia kuzinduliwa kwa chama hicho ni msaada tosha kwa wanafunzi hao wa Kitanzania kuanzia kwenye masomo hadi maisha ya kila siku.
 

Uzinduzi wa umoja huo ulienda sambamba za sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania bara na hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kwa wanafunzi wa Nanchang kusherekea siku yao ya Uhuru wakiwa pamoja.
 

Taarifa kutoka Mo van der Mhando
Nanchang, China. 


Kwa picha zaidi bonyeza hapo
               
                                                                                                                                                



                                    




Mwenyekiti wa Umoja wa wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma Nanchang Given Massawe akikata keki ya miaka 53 ya uhuru wa Tanzania na kuzindua umoja wao





No comments:

Post a Comment