Tuesday 16 December 2014

KENYA YAFUTA USAJILI WA NGOs ZAIDI YA 500


Passengers travelling to Nairobi wait to be searched for weapons in the town of Mandera at the Kenya-Somalia border, 8 December 2014
Kenya imeimarisha usalama kufuatia mashambulio na wanamgambo

Kenya imewafutia usajili mashirika yasiyo ya kiserikali 510 (NGOs), wakiwemo watuhumiwa watano wanaohusishwa na ugaidi, afisa mmoja alisema.

Serikali pia imepiga tanji akaunti zao za benki na kufuta vibali vya kazi vya wafanyakazi wa kigeni.

Hatua hiyo inafuatia mjadala mzito nchini Kenya juu ya mswada mpya tata wa usalama wenye lengo la kupambana na wapiganaji.

Kundi la al-Shabab linalohusishwa na al-Qaeda limezidi kufanya mashambulio Kenya.

Mashirika hayo yalifutiwa usajili wao kutokana na kushindwa kuwasilisha rekodi zao za fedha, alisema Henry Ochido, naibu mkuu wa bodi ya NGOs iliyoteuliwa na serikali, inayosimamia shughuli zao.

Bw Ochido aliiambia BBC, 15 wanatuhumiwa kwa magendo na kufadhili “ugaidi”.

Baadhi walihusishwa na mashambulio mawili ya mabomu ya mwaka 1998 ya balozi za Marekani nchini Kenya na nchi jirani ya Tanzania, alisema.

Bw Ochido alikataa kutaja majina ya mashirika hayo, akisema uchunguzi bado unaendelea.

No comments:

Post a Comment