Wednesday 18 February 2015

BI HARUSI AOLEWA NA MGENI MWALIKWA KWA HASIRA


 Indian bride

Bi harusi mmoja wa India ameolewa na mmoja wa waalikwa katika harusi yake baada ya bwana harusi mtarajiwa kupatwa na kifafa na kuzimia.

Ripoti zilisema bwana harusi huyo mtarajiwa, Jugal Kishore, alikuwa na kifafa na hakumwambia mtarajiwa wake, Indira na familia ya binti huyo.

Wakati Bw Kishore alipopelekwa hospitali, bi harusi huyo mwenye hasira aliamua kutafuta  mume mbadala.

Alimwomba mmoja wa upande wa familia ya shemeji yake, aliyekuwa mwalikwa, kumwoa badala ya mtarajiwa wake. Jambo alilokubali.

Tukio hilo lilitokea mjini Rampur katika jimbo lililo kaskazini mwa India Uttar Pradesh.

Kulingana na gazeti la The Time la India, Bw Kishore, mwenye umri wa miaka 25, alianguka chini mbele ya wageni waalikwa alipotaka tu kumkamata mkono bi harusi wake Indira.

Aliporejea hospitalini, Bw Kishore alimwomba Indira abadili mawazo, akimwambia atabezwa na marafiki na ndugu zake akirudi bila mke, lakini bi harusi huyo alikataa.

Afisa polisi Ram Khiladi aliiambia BBC kuwa awali Bw Kishore na familia yake walikasirishwa na kupeleka malalamiko polisi.

"Lakini kwa kuwa bi harusi huyo kashaolewa, utafanya nini? Familia hizo zimeshatafuta suluhu na wamefuta malalamiko," aliongeza.

No comments:

Post a Comment