Tuesday 10 February 2015

BOBBI KRISTINA 'KUFA' SIKU MOJA NA WHITNEY




http://img2.timeinc.net/people/i/2013/news/130722/bobbi-kristina-600.jpg

Familia ya Bobbi Kristina Brown watachomoa mashine yake ya kupumulia siku ya Jumatano ili Brown aweze kufa siku ileile aliyokufa mama yake Whitney Houston, gazeti la New York Post limeripoti.

Bibi yake Brown na mama yake Whitney, Cissy Houston, alipendekeza wazo hilo mwishoni mwa juma, kulingana na the Post.

Familia inapanga kuchomoa mashine ya Brown ya kupumulia usiku wa Jumanne kuingia Jumatano.

Brown, mwenye umri wa miaka 21, amepooza tangu alipokutwa kwenye bafu nyumbani kwake huko Georgia, Januari 31.

Polisi wanafanya uchunguzi, wakimfutailia zaidi mpenzi wake Nick Gordon, aliyemkuta kwenye bafu hilo.

Inaripotiwa Brown alikuwa na majeraha usoni alipokutwa.

Whitney Houston alifariki dunia Februari 11, 2012, baada ya kuzama kwenye bafu lililojaa maji na baadae mwili wake ukikutwa na dawa za kulevya.

Familia yake na marafiki, akiwemo baba yake Bobbi Kristina, Bobby Brown, wameandaa sala ikiambatana na mishumaa siku ya Jumatatu huko Riverdale.




No comments:

Post a Comment