Monday 2 February 2015

'KABURI' LA MUASI WA LRA UGANDA LAPATIKANA


Ugandan soldiers patrol as part of a mission to combat Lord's Resistance Army (LRA) rebels in Obo in the Central African Republic (CAR) on 11 May 2014
Majeshi ya Uganda yamekuwa yakimsaka LRA, Jamhuri ya Afrika ya Kati 

Jeshi la Uganda limesema limegundua mabaki ya kamanda mwenye cheo kikubwa katika kundi la waasi la LRA.

Okot Odhiambo alikuwa mmoja wa makamanda watano waliopatikana na hatia katika mahakama ya uhalifu wa kivita. 

Inaaminiwa kuwa kaburi lake limegunduliwa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Msemaji wa jeshi la Uganda, Paddy Ankunda aliiambia BBC kuwa majeshi ya Marekani yalikuwa yakifanya uchunguzi wa asidi nasaba (DNA) kujua iwapo ni mabaki ya mwili wa Bw Odhiambo au la.

Kamanda mwengine wa LRA, Dominic Ongwen, alifikishwa mahakama ya ICC wiki iliyopita.

Mkuu wa waasi hao, Joseph Kony, bado hajulikani alipo.

Mkuu wa waasi hao, Joseph Kony, bado hajulikani alipo.


No comments:

Post a Comment