Tuesday 3 February 2015

WABUNGE WAKUBALI MTOTO KUPITIA WATU WATATU



 An embryo

Wabunge wamepiga kura kuunga mkono utengenezaji wa watoto kwa asidi nasaba kutoka wanawake wawili na mwanamme mmoja, katika tukio la kihistoria.

Uingereza sasa itakuwa nchi ya kwanza kuanzisha sheria kuruhusu utengenezaji watoto kwa kutumia watu watatu.

Katika upigaji kura bungeni, wabunge 382 waliunga mkono huku 128 wakipinga mchakato huo unaozuia maradhi yanayohusisha asidi nasaba zinazopita kwa mama kwenda kwa mtoto.

Wakati wa mjadala, mawaziri walisema muundo huo ni “mwanga mwisho wa tanuri la kiza” kwa familia nyingi.

Kura nyingine inatakiwa kupigwa kwenye bunge la House of Lords. Kama kura ikipitishwa basi mtoto wa aina hiyo atazaliwa mwakani.

Inakadiriwa watoto 150 kutoka wazazi watatu huenda wakazaliwa kila mwaka.

No comments:

Post a Comment