Tuesday 17 February 2015

OBASANJO WA NIGERIA ANG'ATUKA CHAMANI



Former Nigerian president Olusegun Obasanjo

Aliyekuwa rais wa Nigeria Olusegun Obasanjo ameng’atuka kutoka chama tawala cha People's Democratic Party (PDP) kabla ya uchaguzi wa Machi 28, akirarua kadi yake ya chama hadharani.

Bw Obasanjo alikuwa mkosoaji mkali wa Rais Goodluck Jonathan, anayetaka kugombea tena kwenye uchaguzi kupitia chama cha PDP.

Bw Jonathan anakabiliwa na changamoto kubwa kutoka mgombea wa upinzani Muhammadu Buhari.

Uchaguzi huo, uliotakiwa kufanyika Februari 14, uliahirishwa kutokana na sababu za kiusalama.

Mchambuzi wa BBC Nigeria alisema uamuzi wa Bw Obasanjo ni pigo kubwa kwa chama cha PDP, ikionyesha mgawanyiko ulioukikumba chama hicho huku ikipambana kuongeza muda wake wa uongozi wa miaka 15.

No comments:

Post a Comment