Tuesday 10 February 2015

MBUNGE AUAWA NA AL-SHABAB SOMALIA



File photo of al-Shabab fighters, February 2011

Mbunge mmoja wa Somalia amepigwa risasi na kufa mjini Mogadishu na wapiganaji wa al-Shabab, maafisa walisema.

Abdullahi Qayad Barre aliuawa karibu na kasri ya rais baada wa watu wenye silaha kumfyatulia risasi kwenye gari lake.

Msemaji wa al-Shabab alisema kundi hilo limehusika na shambulio hilo, na litalenga wabunge wengine.

Kifo cha Barre kimetokea huku kukiwa na ulinzi mkali wakati wabunge walipokusanyika kupiga kura ya kuidhinisha baraza jipya la mawaziri au la.

Ni mfululizo wa mauaji dhidi ya wanasiasa nchini humo.

Takriban wabunge watano waliuawa mwaka jana, lakini Barre ni wa kwanza kuuawa mwaka huu 2015.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na mwandishi wetu                                                                                   

No comments:

Post a Comment